Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 51 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 673 2023-06-20

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza:-

Je ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa skimu za umwagiliaji za Karema na Kabage Mkoani Katavi?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI K.n.y. WAZIRI WA KILIMO alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa kilimo naomba kujibu swali la Mheshimiwa Moshi Selemani Kakoso, Mbunge Jimbo la Mpanda Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha wa 2021/2022 Tume ya Taifa ya Umwagiliaji ilitenga kiasi cha shilingi 84,910,676 kwa ajili ya ukarabati wa mfereji mkuu wa skimu ya umwagiliaji Karema ambapo Mkandarasi amefikia asilimia 80 ya ujenzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali katika mwaka wa fedha 2022/2023 imetenga bajeti ya miradi hiyo ambapo mradi wa umwagiliaji Kabage upo katika hatua ya manunuzi na mradi wa umwagiliaji Karema upo katika hatua za mwisho za usanifu wa bwawa na miundombinu ya umwagiliaji. Ujenzi wa miundombinu katika skimu hizo utakamilika mwaka 2023/2024.