Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Neema Kichiki Lugangira

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA aliuliza:- Je, ni lini Sheria ya Makosa ya Mtandao na Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi Pamoja na Malabo Convention vitahuishwa?

Supplementary Question 1

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru pamoja na majibu mazuri ya Serikali naomba kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.

Kwa kuwa, Malabo convection inaweka msingi wa Makosa ya Mtandao, Ulinzi wa Taarifa Binafsi pamoja na Biashara ya Mtandao, na kwa kutambua fursa zinazotokana na Soko Huru la Afrika la Biashara ya Mtandao; Je, ni lili sasa Serikali italeta azimio hapa Bungeni la kuridhia mkataba huu wa Malabo ili Tanzania isiendelee kuchelewa kupata fursa zinazotokana na soko huru hili la biashara Barani Afrika.

Swali la pili, kwa kuwa tayari Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi imeanza kutumika. Je, ni lini sasa Serikali itatunga kanuni kwa ajili ya sheria hiyo ili kuendelea kulinda Ulinzi wa Taarifa Binafsi ikiwemo changamoto kubwa ya ukatili wa kijinsia mtandaoni? Ahsante.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Neema Lugangira kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Neema Lugangira ambaye amekuwa mdau mkubwa sana katika sekta yetu hii ya mawasiliano.

Kwanza kabisa nianze na swali dogo la pili kuhusiana na Kanuni za Ulinzi wa Taarifa Binafsi. Mheshimiwa Waziri tarehe 6 Mei, 2023 alisaini kanuni hizo ambazo ziko tayari kwa ajili ya kutumika. Kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge anaweza akapata fursa ya kuzipitia na kuona namna gani zinaenda kujibu hoja baadhi ya maeneo ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyataja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza ambalo Mheshimiwa Mbunge ameligusia kuhusu maazimio kuletwa Bungeni. Tayari tuko kwenye mchakato huo na mchakato una hatua kadhaa lakini katika hizo hatua kuna hatua ya kuleta Bungeni. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tuko katika hatua nzuri kabisa na zikishakamilika hatua hizo za awali pale ambapo itahitaji sasa kuileta Bungeni tutaileta kulingana na utaratibu unavyotuelekeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru sana. (Makofi)

Name

Janeth Elias Mahawanga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA aliuliza:- Je, ni lini Sheria ya Makosa ya Mtandao na Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi Pamoja na Malabo Convention vitahuishwa?

Supplementary Question 2

MHE JANETH E. MAHAWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Je, ni lini kanuni za MSA (Media Service Act) zitahuishwa na wadau kushirikishwa ipasavyo?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Janeth Mahawanga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, wiki iliyopita tumepitisha marekebisho ya Media Service Act ambapo tunatarajia Mheshimiwa Rais akishasaini baada ya hapo Mheshimiwa Waziri atatangaza siku ya kuanza kutumika kwake, vilevile tutaanza mchakato wa kuhakikisha kwamba kanuni hizo ambazo zinaendana sambamba na mabadiliko hayo basi zitakuwa zimetungwa na zitapitia katika utaratibu uleule wa kuhakikisha kwamba tunahusisha wadau ili waweze kushiriki katika mchakato mzima na baada ya hapo kanuni zitakuwa tayari kwa ajili ya matumizi. Ahsante.