Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 51 Information, Communication and Information Technology Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 672 2023-06-20

Name

Neema Kichiki Lugangira

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA aliuliza:-

Je, ni lini Sheria ya Makosa ya Mtandao na Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi Pamoja na Malabo Convention vitahuishwa?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Neema Kichiki Lugangira, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekamilisha utungwaji wa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (Personal Data Protection Act, 2022) iliyosainiwa Novemba, 2022 na kutangazwa katika gazeti la Serikali tarehe 2 Desemba, 2022. Sheria hiyo imeanza kutumika rasmi tarehe 1 Mei, 2023.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuweka mazingira wezeshi zaidi ya utekelezaji wa masuala mbalimbali yanayohusiana na TEHAMA nchini ikiwemo kufanikisha kufikia azma ya uchumi wa kidijitali, Serikali kupitia mradi wa Tanzania ya Kidijitali (DTP) inaendelea na zoezi la mapitio ya Sera, Sheria, na Mikataba mbalimbali ya Kikanda na Kimataifa inayohusu TEHAMA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria zinazofanyiwa mapitio kwa ajili ya kuhuishwa ni pamoja na Sheria ya Makosa ya Mtandao ya Mwaka 2015. Vilevile mikataba ambayo utaratibu umeanza kwa ajili ya kuridhiwa ni pamoja na Mkataba wa Malabo.