Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itarudisha huduma za Mahakama za Mwanzo katika Kata ya Kalya Buhingu?

Supplementary Question 1

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba nilulize swali la nyongeza. Kwamba Mahakama ya Mwanzo kule Kalya inaendelea ni kweli. Sasa nilikuwa naomba niishauri Serikali kwamba yule Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo kule Kalya basi aje kwenye Makao Makuu ya Tarafa pale Buhingu kabla jengo hilo halijajengwa la Mahakama ili aendelee kuhudumia wananchi kwa masuala ya sheria, ahsante.

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru naomba nijibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Nashon, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni dhahiri kwamba Makao Makuu haya ya Mgambo na Kalya kuna umbali zaidi ya kilomita 100 na wananchi wamekuwa wakipata tabu kufikia huduma hii. Mahakama yetu ya Tanzania inaridhia maombi ya Mheshimiwa Mbunge kwamba huyo Hakimu aliyeko Kalya aende sasa Mgambo walau tumtafutie Ofisi pale kwa Afisa Tarafa ili huduma, iendelee kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge tunalipokea jambo hili na tunalifanyia kazi na huduma itatolewa. (Makofi)

Name

Mrisho Mashaka Gambo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arusha Mjini

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itarudisha huduma za Mahakama za Mwanzo katika Kata ya Kalya Buhingu?

Supplementary Question 2

MHE. MRISHO M. GAMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Jiji la Arusha limetenga eneo la ekari tano kwenye Kata ya Terrat kwa ajili ya ujenzi wa Mahakama mpya ya mwanzo; je ni lini Serikali itaanza ujenzi wa mahakama hii ya mwanzo kwenye Kata ya Terrat?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mrisho Gambo, Mbunge wa Arusha Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka huu wa fedha ambao tunashukuru Bunge lako tukufu lilitupitishia bajeti ya zaidi ya bilioni 57 fedha za nje pamoja na bilioni 31 fedha za ndani, tumepanga kujenga mahakama zaidi ya 60 na miongoni mwa maeneo ambayo tutakwenda kujenga ni eneo hili la Terrat pale Arusha. Kwa hiyo, Mheshimiwa Gambo kuwa na amani mwaka huu tunajenga Mahakama katika eneo la Terrat.

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itarudisha huduma za Mahakama za Mwanzo katika Kata ya Kalya Buhingu?

Supplementary Question 3

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Je Serikali ina mpango gani wa kujenga Mahakama ya mwanzo eneo la Minjingu?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa nafasi naomba sasa kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Asia Halamga, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Manyara, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mpango wetu huu wa bajeti ya mwaka huu miongoni mwa maeneo ambayo yanahitaji ujenzi wa Mahakama ni pamoja na eneo la Minjingu. Mheshimiwa Asia pamoja na wewe mmekuwa mkikumbusha jambo hili naomba niliarifu Bunge hili Tukufu na wananchi wa Babati Vijijini kwamba tutajenga Mahakama pale Minjingu ili wananchi wapate huduma.

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itarudisha huduma za Mahakama za Mwanzo katika Kata ya Kalya Buhingu?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwa kuwa Mahakama za Usanda na Samuye katika Halmashauri ya Shinyanga zimejengwa toka enzi ya mkoloni. Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati wa Mahakama hizo?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru nijibu swali la Mheshimiwa Mnzava Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Shinyanga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mpango wetu wa Mahakama mwaka huu tunakwenda kujenga Mahakama zaidi ya 38 za Wilaya, Mahakama 60 za mwanzo lakini pia fedha hizi ambazo tumetenga tunakarabati pia Mahakama.

Kwa hiyo, Mheshimiwa Mnzava nipokee Mahakama ambazo umezitaja tutaweka kwenye mpango wetu wa Mahakama ili tuzikarabati.