Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 51 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 671 2023-06-20

Name

Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itarudisha huduma za Mahakama za Mwanzo katika Kata ya Kalya Buhingu?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria, naomba sasa kujibu swali la Mheshimiwa Nashon William Bidyanguze, Mbunge wa Kigoma Kusini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mahakama inaendelea na mipango ya kufanya ujenzi na tayari huduma imerejeshwa kuanzia mwezi Julai, 2022 na mpaka sasa wapo watumishi wanatoa huduma kwa kutumia Ofisi za Kata. Kuanzia mwezi Julai 2022 huduma iliporejea hadi Machi, 2023 jumla ya mashauri 38 yamesajiliwa na kusikilizwa katika Mahakama hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mpango wa ujenzi wa Mahakama, tumepanga kujenga Mahakama ya Mwanzo Mgambo mwaka 2024/2025, ambapo ndiyo Makao Makuu ya Tarafa ya Buhingu. Hivyo, tunatajarajia kuwa wananchi wa Kalya watapata huduma katika Mahakama ya Mwanzo Mgambo. Ahsante.