Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza:- Je, ni lini wananchi 144 wa Kilwa Masoko ambao maeneo yao yalichukuliwa kwa lengo la upanuzi wa Kiwanja cha Ndege watalipwa fidia?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa nafasi ya swali la nyongeza na nitakuwa na maswali mawili ya nyongeza. Nishukuru Serikali kwa hatua hiyo, lakini niombe mchakato wa malipo sasa uharakishwe kwa sababu uthamini huu umefanyika kwa muda mrefu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; kumekuwa na changamoto katika umakini wa uhakiki hususani uliofanyika katika kipindi hiki cha pili ambapo wananchi wengi wamekuwa wakilalamika kwamba wanapunjwa, kucheleweshwa kwa malipo haya na malalamiko mengine mengi. Je, Mheshimiwa Waziri baada ya Bunge hili atakuwa tayari kuambatana nami kwenda Kilwa Masoko kukaa na wananchi hawa kuwasikiliza kero zao na hatimaye kuwapatia majawabu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; Mradi na Mpango huu ni wa muda mrefu, je, ni lini sasa upanuzi na uboreshaji wa Kiwanja cha Ndege Kilwa Masoko utaanza?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ally Mohamed Kassinge, Mbunge wa Kilwa Kusini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa ufuatiliaji wa jambo hili la fidia kwa wananchi wake na Serikali imeendelea kulifanyia kazi. suala la kuambatana naye nimhakikishie nitaambatana naye mara baada ya vikao vya Bunge. Vile vile, nitakuwa na ziara katika Mkoa wa Lindi (Kilwa) Morogoro, Ruvuma pamoja na Iringa. Hivyo, Mheshimiwa Mbunge hata huko Kilwa nitafika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; ni lini hasa upanuzi wa kiwanja utaanza. Ni kwamba tayari tumekuwa na awamu mbili za upanuzi wa kiwanja hiki ambapo awamu ya kwanza ilikuwa kwa ajili ya kutanua ile run way kuweka moramu na sasa hivi tumejenga jengo la abiria lililogharimu takribani milioni 137. Awamu ya pili itafadhiliwa na Benki ya Dunia ambayo iko katika mpango wa Serikali wa mwaka wa fedha ujao. Kwa hiyo, baada ya hapo kiwanja hiki kitakuwa kimekamilika, ahsante sana.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza:- Je, ni lini wananchi 144 wa Kilwa Masoko ambao maeneo yao yalichukuliwa kwa lengo la upanuzi wa Kiwanja cha Ndege watalipwa fidia?

Supplementary Question 2

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Wananchi wanaozunguka Uwanja wa Ndege wa KIA wamekwishafanyiwa tathmini ya baadhi ya maeneo ambayo yanapaswa kupisha Uwanja wa Ndege wa KIA. Swali langu, je, ni lini sasa Serikali itaanza kulipa wananchi hawa fidia?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge Saashisha, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli eneo alilolisema katika uwanja huu Serikali imefanya tathmini na uthamini na kinachoendelea sasa tumeshapeleka lile daftari kwa Mthamini Mkuu wa Serikali, tayari kwa ajili ya malipo na kwenda kupeleka Hazina. Kwa hiyo nimwombe Mheshimiwa Mbunge na wananchi wawe wavumilivu wakati wanasubiri malipo yao, ahsante.