Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 51 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 670 2023-06-20

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza:-

Je, ni lini wananchi 144 wa Kilwa Masoko ambao maeneo yao yalichukuliwa kwa lengo la upanuzi wa Kiwanja cha Ndege watalipwa fidia?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ally Mohamed Kassinge, Mbunge wa Kilwa Kusini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kutekeleza zoezi la ulipaji fidia kwa wananchi waliopisha upanuzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kilwa Masoko, Serikali imehuisha uthamini wa mali za wananchi ndani ya kipindi cha robo ya kwanza ya Mwaka wa Fedha 2022/2023, ambapo idadi ya wananchi iliongezeka kutoka 144 waliofanyiwa uthamini mwaka 2013 hadi kufikia wananchi 438.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Serikali ipo katika hatua za mwisho za maandalizi ya uwekaji wazi Daftari la Fidia (Valuation Report Disclosure) kwa wananchi husika kabla ya kuwasilishwa kwa Mthamini Mkuu wa Serikali kwa idhini, ahsante.