Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukabiliana na ajali za majini?

Supplementary Question 1

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa majibu ya Serikali. Kwa kuwa ajali ni jambo ambalo sometimes haliepukiki, linaweza likatokea wakati wowote. Swali la kwanza; ili kuhakikisha usalama na kuepuka ajali za majini, je, TASAC inachukua hatua gani za kila siku za kuimarisha uokozi kwa ajili ya ajali za majini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; je, Serikali ina mpango gani katika kuwekeza kwenye dhana kama vile boti za mwendokasi, vifaa na kuwawezesha kwa kuwapa utaalam wa uokozi wakati wa ajali za majini?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Asha Abdallah Juma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia Shirika letu la TASAC Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali hususani katika uokozi maeneo ya majini, ziwani pamoja na baharini kwa kuchukua hatua mbalimbali. Hatua ya kwanza, huwa tunatoa elimu kwa wadau wote wanajishughulisha na masuala ya uvuvi baharini ama baharia. Hatua ya pili, kupitia TMA (Mamlaka ya Hali ya Hewa Nchini) ambako tunatoa taarifa ya hali ya hewa kila siku kwa Maziwa yote Ziwa Victoria, Ziwa Tanganyika, Ziwa Nyasa pamoja na Baharini ili kujua mwenendo wa upepo pamoja na hali ya Maziwa hayo na Bahari kwa ujumla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua nyingine, tunafanya uchunguzi wa ajali ili kubaini vyanzo vya ajali hizo na itatusaidia katika ajali nyinginezo zitakazojitokeza na kuzuia zisitokee.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine tumefanya mafunzo kwa Mabaharia kupitia International Maritime Organization na kupewa vyeti (Ithibati) kwa Mabaharia wote ambao wako katika maeneo hayo ya maziwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kuhusu vifaa, kama ambavyo nimejibu kwenye jibu langu la msingi kwamba Serikali katika mwaka wa fedha ujao imetenga takribani bilioni 1.74 kwa ajili ya ununuzi wa boti mbili kwa ajili ya uokozi ambapo boti moja itakuwa kama ambulance katika kutatua changamoto zote ndani ya maziwa na baharini, ahsante.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukabiliana na ajali za majini?

Supplementary Question 2

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa kuwa vifo vingi vinavyotokea Ziwa Tanganyika vinatokana na wananchi kutumia usafiri ambao sio salama, kwa sababu hatuna usafiri wa uhakika kwa maana ya meli. Je, Serikali haioni haja sasa ya kupeleka usafiri wa kisasa Ziwa Tanganyika ili kuokoa vifo vya watu vinavyotokea?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Khenani, Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti yetu ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi iliyosomwa tarehe 22 na 23, tulifanya Commitment kwamba mwaka wa fedha ujao 2023/2024 tunakwenda kujenga na kununua meli mbili za kisasa. Vilevile, hivi karibuni tulikuwa na vikao na Waheshimiwa Wabunge wote wa Mikoa ya Kigoma, Rukwa pamoja na Katavi kuhakikisha kwamba haya ambayo Serikali imefanya commitment katika bajeti, tunakwenda kuyafanya na naamini tutayatekeleza, ahsante. (Makofi)

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukabiliana na ajali za majini?

Supplementary Question 3

MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa mustakabali huo huo kwa jinsi zinavyotokea ajali nyingi si baharini tu hata pale panapotokea barabara inapokutana na reli kuna ajali nyingi sana zinatokea na kusababisha madereva wa treni sasa hivi wanapiga horn usiku kucha na kusababisha watu kutokulala hususani pale treni inapopita ili kuepusha ajali za barabarani zinazotokea. Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka automatic gates katika kila barabara na reli inapokatiza ili kuondoa ajali na kutokupiga horn usiku zinazowafanya watu kukosa usingizi?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Nyongo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kumekuwa na changamoto kubwa sana kati ya maeneo ambapo barabara inapita na reli inapita. Kwa kutambua hilo, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kupitia Shirika letu la Reli Nchini, tumetangaza tenda kwa ajili nya kuweka mifumo mipya automatic systems ambayo itakuwa ni gate way inajifunga na kufunguka automatic. Vile vile, tenda hii mwisho wa ku–submit ni kesho.

Kwa hiyo, wale wote ambao wako interested na ni international tender, wanakaribishwa kuomba ili tuweze kutengeneza mifumo yote na maeneo yote ya mapitio kati ya barabara na reli, ahsante.