Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 51 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 669 2023-06-20

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kukabiliana na ajali za majini?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Asha Abdullah Juma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) imeanza kutekeleza Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Kikanda cha Uratibu wa Shughuli za Utafutaji na Uokoaji Majini (Regional Maritime Rescue Coordination Center – MRCC) kupitia mradi unaoendelea katika Ziwa Victoria na vituo vidogo vinne vya uratibu wa shughuli za utafutaji na uokoaji majini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mradi huu unatekelezwa kwa fedha za ndani pamoja na mkopo kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) ambapo katika mwaka 2023/2024 umetengewa Shilingi bilioni 1.74. Aidha, kupitia mradi huo zitanunuliwa boti tatu kwa ajili ya shughuli ya utafutaji na uokoaji ambazo kwa sasa zipo katika hatua za manunuzi, ahsante.