Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. ALLY A. J. MLAGHILA aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa barabara ya kutoka Ibanda hadi Itungi Port (kilometa 25) utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY A. J. MLAGHILA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niishukuru sana Serikali ya Chama cha Mapinduzii kupitia Rais wetu Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa ujenzi wa barabara hii na kwamba sasa imeanza. Sasa, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; je, Serikali imejiridhisha na uwezo wa Mkandarasi huyu mpaka kumpata maana inachoonekana sasa ni kwamba mkandarasi anasuasua sana tangu alipopewa ile site?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, wananchi wote ambao wamepitiwa na barabara hiyo tangu miaka mitano iliyopita waliambiwa wasiendeleze maeneo yao na mpaka sasa hivi hawajalipwa maeneo yao na bado hawajapewa hata kiasi chochote au karatasi lolote linaloonesha kwamba wanaweza kulipwa kiasi fulani. Je, ni lini Serikali itawalipa wananchi wanaopitiwa na barabara hii pesa zao za fidia?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ally Anyigulile Jumbe Mlaghila, Mbunge wa Kyela, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Kyela kwamba Mkandarasi ambaye amepewa kazi hii ana uwezo wa kutosha ndiyo maana amepewa kazi hiyo. Vile vile, ni mkandarasi ambaye alifanyiwa due diligence kwa maana ya kuangalia uwezo wake wa kifedha kwa maana ya mtaji lakini pia na vifaa vya kufanyia kazi hiyo. Kwa hiyo, tunaamini uwezo huo anao na ataijenga hiyo Barabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake la pili la fidia. Ni kweli wananchi hawa bado hawajalipwa fidia, lakini nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Kyela kwamba uthamini ulishakamilika na majedwali ya malipo yalishakamilishwa na tayari Wizara ilishapeleka uthamini kwa maana ya gharama watakazolipwa ambayo ni bilioni 1.734 kwa wananchi wanaostahili kulipwa, hususani wale ambao watapisha ujenzi huu na watalipwa kwa mujibu wa Sheria yetu ambayo tunaituma kwa watu wanaopisha ujenzi wa barabara, ahsante.

Name

Kabula Enock Shitobela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALLY A. J. MLAGHILA aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa barabara ya kutoka Ibanda hadi Itungi Port (kilometa 25) utaanza?

Supplementary Question 2

MHE. KABULA E. SHITOBELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, je, ni lini ujenzi wa Barabara ya Hungumalwa – Kwimba kwenda Magu utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shitobela, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara aliyoitaja ya Hungumalwa – Ngudu – Bukwimba hadi Magu ni barabara ambayo kumekuwa na watu wengi ambao wameipigia kelele sana. Hata hivyo, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, katika mwaka wa fedha ambao bajeti tayari imeshapitishwa barabara hii imetengewa fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami kwa sababu usanifu ulishakamilika tayari, ahsante.

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Primary Question

MHE. ALLY A. J. MLAGHILA aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa barabara ya kutoka Ibanda hadi Itungi Port (kilometa 25) utaanza?

Supplementary Question 3

MHE MASHIMBA M. NDAKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara ya Njia Panda - Ikungu kwenda Malampaka kilometa 14 au 15 inajengwa kwa lami, leo ni mwaka wa sita lakini zimejengwa kilometa nne tu. Sasa naomba kujua ni lini Serikali itatenga kiasi cha pesa cha kutosha ili kuweza kukamilisha ujenzi wa barabara hiyo ambayo ni muhimu kuunganisha Mkoa wa Simiyu na Kituo kikubwa cha SGR pale Malampaka?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba nikubaliane na Mheshimiwa Mbunge kuhusu swali lake la muhimu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara aliyoitaja ni kweli ndio barabara ambayo inaunganisha SGR, Mkoa wa Simiyu na hata watu ambao wanaweza kwenda na ndio kituo sahihi na hiyo barabara ndiyo inayounga. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, Serikali itafanya kila kinachowezekana kuhakikisha kwamba ahadi iliyoitoa ya kujenga hizo kilometa 14 ambazo bado kilometa 10 tunaikamilisha ili kuhakikisha kwamba Kituo cha Malampaka kitakuwa ni muhimu sana kwa wananchi wa Maswa na Bariadi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, Serikali inafahamu na itahakikisha kwamba inaijenga hiyo barabara kwa kiwango cha lami, ahsante.