Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 51 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 668 2023-06-20

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. ALLY A. J. MLAGHILA aliuliza:-

Je, ni lini ujenzi wa barabara ya kutoka Ibanda hadi Itungi Port (kilometa 25) utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ally Anyigulile Jumbe Mlaghila, Mbunge wa Kyela, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkataba wa ujenzi wa Barabara ya Ibanda – Kajunjumele – Kiwira/Itungi Port yenye urefu wa kilometa 32 ulisainiwa rasmi mnamo tarehe 27 Desemba, 2022 na kupewa kibali cha kuanza ujenzi mnamo tarehe 31 Machi, 2023. Kwa sasa Mkandarasi yupo eneo la mradi anaendelea na ujenzi wa Kambi za Mkandarasi na Msimamizi wa mradi ikiwa ni pamoja na maandalizi mengine kwa ajili ya kuanza ujenzi, ahsante.