Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza: - Je, ni lini Halmashauri ya Sikonge itapatiwa shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya kujenga Vituo vya Afya Ipole, Kipanga na Usunga?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana majibu ya Serikali yamekuwa mazuri. Lakini kwa hali ya Jimbo la Sikonge ilivyo, kilometa za mraba 27,873, kuna wananchi wanatembea kilomita 70 mpaka kilometa 100 kufikia kituo cha afya cha karibu; je, Serikali haioni kwamba Wilaya au Jimbo kama la kwangu wanatakiwa waweke kipaumbele maalum ili watu wasiwe wanatembea kilomita 100 kufata kiyuo cha afya?

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili hizo fedha ambazo nimeuliza mimi bilioni 1.5 ni ela kidogo sana kwa Serikali; je, lini watatupatia hizo ela ili tuanze na hivyo vituo vitatu tulivyopendekeza?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Kakunda Mbunge wa Sikonge, la kwanza la Serikali kuona umuhimu. Serikali inaona umuhimu wa kujenga vituo vya afya kote nchini na ndio maana Serikali hii ya Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ilijenga vituo vya afya 234 kwa kutumia zaidi ya bilioni 117 kwa ajili ya kupeleka huduma karibu na wananchi. Tutakaa kuona ni mipango ipi iliyowekwa katika mwaka wa fedha 2023/2024 kwa ajili ya kujenga vituo vya afya katika Wilaya ya Sikonge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye swali la pili, tutaangalia kadri ya upatikanaji wa fedha. Tutawasiliana na wenzetu wa Wizara ya Fedha kuona tunapataje fedha hii kwa ajili ya kusogeza huduma karibu kule Jimboni Sikonge.

Name

Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza: - Je, ni lini Halmashauri ya Sikonge itapatiwa shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya kujenga Vituo vya Afya Ipole, Kipanga na Usunga?

Supplementary Question 2

MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Mwaka huu wa fedha unaoisha 2022/2023 Serikali ilitenga milioni 500 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Kituo cha Afya kwenye Kata ya Igusule, Jimbo la Bukene Halmashauri ya Wilaya ya Nzega. Sasa, ukizingatia kwamba bado siku chache mwaka huu uishe;

Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu kupeleka fedha hizi sasa milioni 500 ambazo ilizitenga kwenye Kata ya Igusule ili ujenzi wa Kituo cha Afya uanze?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nitakaa na Mheshimiwa Zedi kuona hizi milioni 500 zilizotengwa ni hatua gani imefikiwa kwa ajili ya kuzipeleka kwa ajili ya kuanza ujenzi wa kituo cha afya kule Igusule, Jimboni Bukene.

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza: - Je, ni lini Halmashauri ya Sikonge itapatiwa shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya kujenga Vituo vya Afya Ipole, Kipanga na Usunga?

Supplementary Question 3

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru. Niipongeze Serikali kwa kujenga vituo 234 vya afya nchini kikiwemo kituo cha kisasa kabisa pale katika Kata ya Kinondoni ambacho tayari kimeanza kufanya kazi. Tatizo ni uhaba wa madaktari na wauguzi;

Je, Serikali haioni umuhimu sasa wa kuhakikisha vituo hivi vipya ambavyo vimejengwa vinapata na kuondolewa tatizo la kuwa na madaktari na wauguzi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Tarimba la kupata madaktari na wauguzi katika kituo cha afya Kinondoni. Jitihada za Serikali ya Awamu hii ya Sita katika kuhakikisha vituo vya Afya vyote vilivyojengwa na vilivyopo vinapata watumishi wa kutosha imefanyika kubwa katika mwaka wa fedha huu 2022/2023 kwa kuajiri watumishi wa afya 8070. Tayari watumishi hao wameanza kupangiwa maeneo yao ya kazi ikiwemo Halmashauri ya Kinondoni. Hivyo basi nimtake Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni kuhakikisha kati ya wale ajira mpya atakao wapokea aweze kuwapangia katika vituo hivi vya afya ambavyo vimejengwa kwa fedha nyingi iliyotolewa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza: - Je, ni lini Halmashauri ya Sikonge itapatiwa shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya kujenga Vituo vya Afya Ipole, Kipanga na Usunga?

Supplementary Question 4

MHE. MASACHE N. KASAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Kituo cha Afya cha Matwiga, Isangawana na Mafyeko vilipata milioni mia tatu kila kituo na ujenzi wake ulishaanza;

Je, ni lini Serikali itatoa fedha ili vituo hivyo viweze kumalizika na baadaye wananchi waweze kupata huduma?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Masache Kasaka Mbunge wa Lupa; changamoto iliyojitokeza kule Wilayani Chunya ilikuwa kwamba fedha ilipelekwa na Serikali kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya kimoja. Wao wenyewe walikaa kwenye Baraza la Madiwani wakaamua kugawanya fedha ile na kuanzisha ujenzi wa vituo vya afya viwili. Ni mategemeo yangu kwamba walipopitisha maamuzi yale walijua wana mapato ya kutosha kwa ajili ya kumalizia vituo vya Afya hivi vya Isangawana na Mpepo kule. Lakini nitakaa na Mheshimiwa Kasaka kuona ni namna gani tunaweza tukakaa, tukazungumza na Mkurugenzi wa Halmashauri ili waweze kumalizia maeneo haya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mgogoro ule ulianzishwa na wao wenyewe Madiwani kwa kugawanya fedha iliyotolewa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya kimoja.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza: - Je, ni lini Halmashauri ya Sikonge itapatiwa shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya kujenga Vituo vya Afya Ipole, Kipanga na Usunga?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona. Kituo cha Afya cha Mafiga ni kituo kikubwa ambacho hasa kinatoa huduma kwa akinamama wajawazito. Je, ni lini Serikali itatoa hela ya kumalizia jengo la upasuaji?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itatoa fedha kwa ajili ya umaliziaji wa Kituo hiki cha Afya Mafiga kadri ya upatikanaji wake, lakini tutaangalia katika mwaka wa fedha 2023/2024 kama kuna fedha imetengwa ili iweze kupelekwa mara moja kwa ajili ya kumalizia kituo hicho.