Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sylivia Francis Sigula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE.SYLIVIA F. SIGULA K.n.y. MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kumalizia ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Kizazi?

Supplementary Question 1

MHE. SYLIVIA F. SIGULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niipongeze Serikali na niishukuru kwa majibu mazuri. Tunashukuru kwa hizo milioni mia tano kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, Wilaya ya Kibondo kata ya Nyaruyoba hakuna Kituo cha Afya na wananchi wanahangaika. Tumeahidiwa milioni 200 kwa ajili ya ujenzi wa wodi.

Je, ni lini Serikali itatuletea milioni 200 hizo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini swali la pili Wilaya ya Buhigwe kata ya Mbanga na Kata ya Mhinda hakuna Vituo vya Afya, wananchi wanatembea umbali mrefu kupata huduma.

Je, ni lini Serikali itajenga Vituo vya Afya katika kata hizo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nijibu maswali mawili ya nyongeza yaliyoulizwa na Mheshimiwa Sigula; la kwanza hili la Nyaruyoba kule Wilayani Kibondo milioni mia mbili, tutakaa na Mheshimiwa Mbunge ili tuweze kuwasiliana na idara ya afya katika Ofisi ya Rais TAMISEMI kuona fedha hizi zilizo ahidiwa zinaweza kwenda mara moja kwa ajili ya kuanza ujenzi wa kituo cha afya kule Wilayani Kibondo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye swali lake la pili, tutafanya tathmini kule Wilayani Buhigwe na kuona vituo hivi vya afya alivyoviomba Mheshimiwa Sigula kama vina kidhi vigezo vya kuweza kupandishwa hadhi na kuwa vituo vya afya ili tuweze kutenga fedha katika mwaka wa fedha unaofata kwa ajili ya kuanza ujenzi wake mara moja.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE.SYLIVIA F. SIGULA K.n.y. MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kumalizia ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Kizazi?

Supplementary Question 2

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kata ya Kiwila katika Jimbo la Rungwe ni kata yenye wakazi wengi sana na kituo cha afya bado hakija malizika.

Je, ni lini Serikali mtatuongezea nguvu ili tuweze kumaliza kituo kile na kusaidia wananchi wa kata ile?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwakagenda kuhusu kata ya Kiwila kumaliziwa kituo chao cha afya. Nitakaa naye kuweza kujua ni majengo yapi ambayo bado hayajakamilika na kuhakikisha kwamba tunaona ni mipango ipi iliyotengwa na Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe. Lakini vile vile sisi katika Ofisi ya Rais, TAMISEMI tutaona kwenye bajeti ya mwaka 2023/2024 ni kiasi gani kimetengwa kwa ajili ya Kituo hiki cha Afya Kiwila ili fedha hizo ziweze kwenda mara moja kwa ajili ya kumalizia majengo hayo.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE.SYLIVIA F. SIGULA K.n.y. MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kumalizia ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Kizazi?

Supplementary Question 3

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa nafasi. Mbulu Vijijini wananchi wamechanga na wamejenga kwenye Kata ya Geterei OPD kama Kituo cha Afya, na Kata ya Maseda vilevile; je, lini mtapeleka fedha kuunga juhudi za wananchi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niwapongeze Mheshimiwa Mbunge Flatei Massay vile vile na Mheshimiwa DC wake pale Ndugu Heri James kwa jitihada kubwa ambazo wanazifanya kwa ajili ya kusukuma gurudumu la maendeleo kwa kuhamasisha wananchi kujenga miundombinu ya afya. Nitakaa na Mheshimiwa Flatei kuona ni mipango gani ambayo imewekwa kwetu katika Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa ajili ya kumalizia vituo vya afya ambavyo amevitaja.

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE.SYLIVIA F. SIGULA K.n.y. MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kumalizia ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Kizazi?

Supplementary Question 4

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Mwaka mmoja nyuma Waheshimiwa Wabunge wote tulitakiwa kutoa vipaumbele vya ujenzi wa Vituo vya Afya kwenye majimbo yetu. Mimi Mbunge wa Jimbo la Kibaha Vijijini ni miongoni na nilipewa Kituo cha Afya cha Kata ya Ruvu, lakini hadi leo hakuna kinachoendelea; je, nini kauli ya Serikali kwenye kuanzisha ujenzi wa kituo hicho?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha wa 2021/2022 Serikali ilijenga vituo vya afya 234 kote nchini, na hii ni commitment kubwa ya Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha tunapata vituo vya afya kwenye maeneo yote ya kimkakati hapa nchini ikiwemo kule Kibaha Vijijini alipotaja Mheshimiwa Mwakamo. Tutakaa tuone katika mipango iliyowekwa mwaka 2023/2024 wa fedha, ni kiasi gani kimetengwa kwa ajili ya Kibaha Vijini ili kqenda kujenga kituo cha afya hicho cha kimkakati ambacho amekitaja Mheshimiwa Mwakamo.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE.SYLIVIA F. SIGULA K.n.y. MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kumalizia ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Kizazi?

Supplementary Question 5

MHE.BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru. Jimbo la Bunda limekuwa na kituo cha muda mrefu cha zamani kinaitwa Ikizu, na kimechaka sana, na Serikali imetoa ahadi ya kukarabati vituo vya zamani vya afya;

Je, ni lini Kituo cha Ikizu kitakarabatiwa kwa ahadi ya Serikali?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nitakaa na Mheshimiwa Getere ili kuweza kuona ahadi hiyo ya Serikali ilitolewa lini ili tuweze kuifatilia vizuri kwenye idara husika ambayo ilitoa ahadi hiyo na tuweze kuhakikisha tunapata fedha kwa ajili ya kukarabati kituo cha afya hicho alichokitaja Mheshimiwa Getere.