Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatenga bajeti ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya pamoja na Vituo vya Afya Misenyi?

Supplementary Question 1

MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nipongeze kwa majibu mazuri ya Serikali, na ni kweli majengo saba yamejengwa. Naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, katika majengo hayo hatuna wodi ya watoto, akina baba, akina mama pamoja na theatre;

Je, ni lini sasa wodi hizo zitajengwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili, ili hospitali hiyo iendane na kutoa huduma ya haraka kama ambavyo speed ya ujenzi imeenda inahitaji kuunganishwa na barabara ya lami ambayo iliahidiwa na kiongozi wa kitaifa.

Je, na barabara hiyo ambayo iko chini ya TARURA ni lini itajengwa kwa kiwango cha lami kuelekea katika hospitali iweze kutumika itakapo funguliwa?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Kyombo, la kwanza hili la kutokuwa na wodi ya watoto, akina baba na theatre vile vile katika Hospitali ya Wilaya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo nilikuwa nimeshasema kwenye majibu yangu ya msingi kwamba Serikali imetenga shilingi milioni 800 katika mwaka wa fedha wa 2023/2024 ambayo itakwenda kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa Hospitali hii ya Wilaya ya Misenyi na watapata wodi ya watoto, baba na vilevile theatre. Ni lengo la Serikali hii ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhakikisha kwamba miundombinu katika sekta ya afya ipo ya kutosha kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi wa nchi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye swali lake la pili la barabara inayounganisha hospitali. Barabara hii ina urefu kama wa kilomita nne kutoka kwenye barabara kuu inayokwenda Mtukula ambayo ni barabara ya TANROADS. Hivyo naomba nichukue nafasi hii mbele ya Bunge lako Tukufu kumwelekeza Meneja wa TANROADS Mkoa wa Kagera kwenda kufanya tathmini ya barabara hii na kuiweka katika mipango yetu kwa ajili ya kutafuta fedha na kuweza kuijenga ili wananchi waweze kufika hospitali kupata huduma za afya kwa wakati.

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatenga bajeti ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya pamoja na Vituo vya Afya Misenyi?

Supplementary Question 2

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Kwanza niipongeze Serikali ya Chama Cha Mapinduzi kwa kutujengea Vituo vya Afya kwenye tarafa tatu. Tuna tarafa nne Wilaya ya Kilindi lakini tuna Tarafa moja ya Kimbe haina kituo cha afya na umbali kutoka tarafa hiyo hadi Makao Makuu ya Wilaya ni takribani kilomita 120;

Je, nini mpango wa Serikali wa kujenga kituo cha afya kwenye tarafa hiyo? Ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nijibu swali la Kigua Mbunge wa Kilindi, kwamba Tarafa ya Kimbe haina na kituo cha afya. Serikali imetenga mwaka wa fedha uliopita zaidi ya bilioni 117 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya vya kimkakati kote nchini ambapo vingine vilikwenda kwa Mheshimiwa Kigua kule Kilindi. Tutakaa na Mheshimiwa Kigua kuona hii Tarafa ya Kimbe nayo tunafanyaje ili iweze kutengewa fedha kupata ujenzi wa kituo cha afya kama vile kata ya kimkakati ili hizi kata zote zinazozunguka tarafa hii ziweze kupata huduma nazo za afya.

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatenga bajeti ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya pamoja na Vituo vya Afya Misenyi?

Supplementary Question 3

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa. Tunaishukuru sana Serikali kwa kutujengea Kituo cha Afya cha Uru Kusini na kinakaribia kinakamilika;

Je, Serikali ina mpango gani kupeleka vifaa na wahudumu ili wananchi waanze kupata huduma?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali katika mwaka huu wa fedha 2022/2023 imeajiri watumishi wa afya wapatao 8,000 ambapo wengine watapangiwa katika Halmashauri ya Moshi Vijijini anapotoka Prof. Ndakidemi kule. Lakini vile vile katika mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali imeweka kwenye bajeti shilingi bilioni 112 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba. Vitakapo nunuliwa tutahakikisha na Moshi Vijijini napo kwa Mheshimiwa Profesa Ndakidemi nao wanapata vifaa tiba hivi.

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatenga bajeti ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya pamoja na Vituo vya Afya Misenyi?

Supplementary Question 4

MHE. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Wilaya ya Muleba ni Wilaya kongwe hapa nchini lakini haina hospitali ya Wilaya na mwaka jana Mheshimiwa Rais alitupatia fedha kuanza ujenzi wa hospitali hiyo.

Je ni lini sasa ujenzi utakamilika wa Hosoitali ya Wilaya ya Muleba?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa Hospitali hizi za Wilaya huwa unaenda kwa awamu na fedha hutolewa kwa awamu.

Awamu ya kwanza hutolewa milioni mia tano ama wakati mwingine bilioni moja kwa ajili ya kuanza ujenzi huo; na katika kila mwaka wa fedha Serikali hutenga fedha kwa ajili ya kuendelea na kumalizia ujenzi wa Hospitali hizi za Wilaya. Nimtoe mashaka Mheshimiwa Mbunge, tutakaa na wenzetu wa Wizara ya Fedha kuona katika mipango yao wameweka kiasi gani katika mwaka wa fedha unao fata ili ziweze kwenda Muleba kule kwa ajili ya ukamilishaiji wa Hospitali hii ya Wilaya.

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatenga bajeti ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya pamoja na Vituo vya Afya Misenyi?

Supplementary Question 5

MHE. ENG. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi. Tarafa ya Balangaralu Makao Makuu yake yako Kata ya Balanga na pale hakuna Kituo cha Afya.

Je, Serikali ni lini itapeleka fedha ili kituo cha afya kijingwe pale?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itapeleka fedha katika Tarafa aliyoitaja Mheshimiwa Hhayuma kule Hanang kwa kadri ya upatikanaji wa fedha. Tutaangalia katika mipango iliyopo katika mwaka wa fedha unaofata 2023/2024 kuona kama fedha yoyote imetengwa kwa ajili ya kwenda Halmashauri ya Wilaya ya Hanang ili tuweze kuhakikisha inaenda haraka kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya.