Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 51 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 664 2023-06-20

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatenga bajeti ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya pamoja na Vituo vya Afya Misenyi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Florent Laurent Kyombo, Mbunge wa Jimbo la Nkenge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha wa 2021/2022 na hadi kufikia Mei, 2023 kiasi cha shilingi bilioni 1.5 zimekwishatumika katika ujenzi wa majengo saba ya Hospitali ya Wilaya ya Misenyi na kiasi cha shilingi milioni 500 kilitengwa kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya cha kimkakati cha Kanyigo kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Misenyi. Aidha, katika mwaka wa fedha wa 2023/2024, Serikali imetenga shilingi milioni 800 kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Misenyi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenge bajeti kwa ajili ya ujenzi na ukamilishaji wa miundombinu msingi katika hospitali na vituo vya afya kote nchini vikiwepo vya Halmamashauri ya Wilaya ya Misenyi.