Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA atauliza: - Je, ni lini mradi wa maji Kata za Kaengeza na Kanda Sumbawanga Vijijini itakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, nilitaka kujua ni lini sasa Serikali itapeleka fedha kwenye mradi uliochukua muda mrefu mradi wa Inkana Isarye ulioko Nkasi Kusini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini swali la pili, nilitaka kujua ni lini sasa Serikali itakamilisha mradi wa kutoa maji katika Ziwa Tanganyika na kusambaza Mkoa wa Rukwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Awali ya yote nipende kumpongeza Mheshimiwa Bupe Mwakang’ata Mbunge wa Viti Maalum kwa ufatiliaji wake mzuri na nipende kuhakikishia malipo ya mradi huu ambao umechukua muda mrefu ni mmoja wa vipaumbele vya Wizara kuhakikisha miradi yote inakamilika. Lengo la kupata maji bombani linatimia kwa sababu tunahitaji kuona tunapunguza umbali mrefu wananchi wa kutembea, vilevile kusambaza maji kutoka Ziwa Tanganyika ni moja ya vipaumbele vya Wizara. Mheshimiwa Bupe hili nalo pia Wizara tunalipa uzito na tutahakikisha maeneo yote ya Nkasi Kusini na Kaskazini kote tuweze kuyafikia na miradi iweze kukamilika.

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA atauliza: - Je, ni lini mradi wa maji Kata za Kaengeza na Kanda Sumbawanga Vijijini itakamilika?

Supplementary Question 2

MHE DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Jimbo la Njombe Mjini pamoja na kwamba linaonekana ni jimbo la mjini, uhalisia ni kwamba lina vijiji vingi sana ambavyo bado havina huduma ya maji kama Uliwa, Ihanga, Mikongo, Liwengi na Mtira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hawajaingizwa katika mpango mkubwa wa maji wa P4R. Serikali ina mpango gani kuhakikisha kwamba na vijiji hivi vinapata huduma hii ya maji safi na salama?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deodatus Phillip Mwanyika Mbunge wa Njombe Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo yote haya aliyoyataja Mheshimiwa Mbunge ni kweli. Mheshimiwa Mbunge nikupongeze hili mimi na wewe tumeshalijadili na tayari tumeanza kulifatilia. Maeneo ambayo hayata nufaika na mradi wa P4R ambao tunautekeleza kwa kutimiza vigezo vya masharti ya namna ambavyo unatekelezeka yatafanyiwa huduma kwa kupitia fedha za mfuko wa maji lakini vile vile fedha nyingine ambazo tunazipata kwenye namna nyingine ya upatikanaji wa fedha ndani ya Wizara.

Mheshimiwa Mbunge, nikuondoe hofu, kwa maeneo ambayo P4R haitafika haimaanishi hatutaweza kutekeleza miradi. Tutatekeleza miradi na wananchi watapata maji safi na salama ya kutosha na wote wataendelea kunufaika na kutuliwa ndoo kichwani.