Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 48 Water and Irrigation Wizara ya Maji 637 2023-06-14

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA atauliza: -

Je, ni lini mradi wa maji Kata za Kaengeza na Kanda Sumbawanga Vijijini itakamilika?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bupe Nelson Mwakang’ata, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kata ya Kaengesa ina vijiji vinne ambapo katika mwaka 2022/2023, Serikali inaendelea kutekeleza mradi wa maji Mkunda Group utakaohudumia vijiji vya Mkunda, Kaengesa A na Kaengesa B. Mradi huo unatarajia kukamilika mwezi Septemba, 2023 na wananchi Kijiji cha Mkunda wameanza kupata huduma ya maji. Kwa Kijiji cha Itela, Serikali itafanya usanifu na kujenga mradi wa maji katika mwaka wa fedha 2023/2024.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa Kata ya Kanda yenye vijiji vinne, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali inaendelea kutekeleza mradi wa maji utakaohudumia vijiji vya Lula na Chitete. Vijiji vinavyobaki vya Lyapona A na Lyapona B usanifu utafanyika katika mwaka wa fedha 2023/2024 na miradi kujengwa.