Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE K.n.y. MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: - Je, ni lini changamoto ya upatikanaji maji Mji wa Mlowo itatatuliwa?

Supplementary Question 1

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali nataka nimwombe Mheshimiwa Naibu Waziri, Je, yupo tayari kuongozana na mimi Mbunge wa Jimbo la Mbozi kwenye mji wa Mlowo kuangalia hivyo vyanzo vya maji na kuhakikisha kwamba yote aliyosema yataenda kutekelezwa kwa wakati?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa George Ranwell Mwenisongole Mbunge wa Jimbo. Awali ya yote nipokee pongezi lakini Mheshimiwa Mbunge na wewe nakupongeza na ninakusihi tuendelee kushirikiana. Ufuatiliaji wako wa karibu ndio matunda ya miradi hii kufika hatua hizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kuongozana Mheshimiwa Mbunge, kama tulivyoongea ulipokuja Wizarani kufuatilia miradi hii, niko tayari na tutakwenda kuhakikisha miradi hii inatekelezwa kwa wakati.

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE K.n.y. MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: - Je, ni lini changamoto ya upatikanaji maji Mji wa Mlowo itatatuliwa?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. PIUS STEPHEN CHAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa hii nafasi kuuliza swali la nyongeza. Katika Jimbo la Manyoni Mashariki kuna mradi wa maji wa Kintiko wa vijiji 11 Mkandarasi alisaini Mkataba mwezi Februari mwaka huu lakini mpaka sasa hivi kazi haijaanza. Nini kauli ya Serikali kuhakikisha kwamba Mkandarasi anaanza kazi ya kumalizia huu mradi? Ahsante sana.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Chaya Mbunge wa Jimbo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi huo anaongelea Mheshimiwa Mbunge ni kweli lakini nampongeza kwanza Mkandarasi ameanza kufanya kazi zile za awali na kinachosababisha hajaanza anasubiria advance payment lakini ninamsihi pale anapoweza kuendelea kufanya aendelee kwa sababu malipo haya yako mwishoni na yeye pia atalipwa kwa sababu tumeshapokea andiko lake.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE K.n.y. MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: - Je, ni lini changamoto ya upatikanaji maji Mji wa Mlowo itatatuliwa?

Supplementary Question 3

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Serikali imenunua magari ya kuchimba maji katika kila Mkoa na yako chini ya DDCA. Je, ni lini yatakuwa chini ya Wahandisi wa maji wa Mikoa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Yahaya Omary Massare kuhusiana na magari ya uchimbaji visima kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwa sasa hivi magari haya yako chini ya DDCA tayari taratibu za ndani za kiwizara zinaendelea wakati wowote mambo yote yatakaa sawa kwa RMs wa Mikoa yote.

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE K.n.y. MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: - Je, ni lini changamoto ya upatikanaji maji Mji wa Mlowo itatatuliwa?

Supplementary Question 4

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Naomba kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri wa Maji. Wilaya ya Mbongwe ina maeneo yaliyo na changamoto ya maji. Je, ni lini Mbogwe mtatupa gari hilo la kuweza kuchimbia visima ili wananchi waweze kupata maji safi na salama kupitia hayo, magari mliyoleta?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Maganga Mbunge wa Mbogwe kama ifuatavuyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Maganga anafatilia sana na hili tumeshaongea. Mheshimiwa Maganga naomba uiamini Wizara, mimi mwenyewe na wewe tutakwenda kuhakikisha kazi zinakwenda kuanza kwa wakati na visima vitachimbwa.

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE K.n.y. MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: - Je, ni lini changamoto ya upatikanaji maji Mji wa Mlowo itatatuliwa?

Supplementary Question 5

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Je, ni lini Serikali itatusaidia changamoto ya maji katika kata ya Kasokola katika Manispa ya Mpanda?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Awali ya yote nipende kumpongeza Mheshimiwa Mbunge Kapufi kwa kweli umekuwa ukifuatilia kata hii na nikuhakikishie katika maeneo ambayo tunakwenda kupeleka jitihada ni pamoja na kata hiyo uliyoitaja kuhakikisjha wananchi nao wananufaika na hekima kubwa anayotumia Mheshimiwa Rais wetu kuhakikisha wanawake tunawatua ndoo kichwani.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE K.n.y. MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: - Je, ni lini changamoto ya upatikanaji maji Mji wa Mlowo itatatuliwa?

Supplementary Question 6

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Je, Serikali ina mpango gani kutuongezea visima virefu Mkoa wa Simiyu tukiwa tunasubiri mradi wa Ziwa Victoria?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nampongeza Mheshimiwa Esther Midimu kwa kweli naye pia ni mfatiliaji mzuri lakini nikupongeze kwa sababu ulishiriki katika usainishaji wa mradi ule mkubwa wa maji kutoka Ziwa Victoria lakini masuala haya ya uchimbaji wa visima pia yatakwenda sambamba na maji kuvutwa kutoka Ziwa Victoria na visima hivi vyote mwaka ujao wa fedha tutajitahidi maeneo mengi kuyafikia.