Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 48 Water and Irrigation Wizara ya Maji 636 2023-06-14

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE K.n.y. MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: -

Je, ni lini changamoto ya upatikanaji maji Mji wa Mlowo itatatuliwa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Juliana Daniel Shonza, Mbunge wa Viti maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua adha ya maji wanayoipata wakazi wa Mji wa Mlowo ambapo hali ya upatikanaji wa huduma hiyo ni asilimia 49. Katika kukabiliana na hali hiyo, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali inatekeleza miradi mitatu ambayo ni Mradi wa Uboreshaji Huduma ya Maji Mlowo ambao umekamilika mwezi April 2023, na inaendelea na utekelezaji wa Mradi wa Upanuzi wa Mtandao wa maji Vwawa-Mlowo na Mradi wa Ukarabati wa Chanzo cha Maji Mwansyana na Mlowo. Miradi hii inatarajia kukamilika mwezi Septemba, 2023 na kuongeza hali ya upatikanaji wa huduma ya maji Mlowo kufikia asilimia 65.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile, Serikali imepanga kujenga miradi mingine miwili ambayo ni Mradi wa Maji kupitia chanzo cha Mto Mafumbo, na Mradi wa Maji wa Vwawa-Mlowo na Tunduma kupitia chanzo cha Mto Momba. Miradi hiyo ipo kwenye hatua ya manunuzi ya Wakandarasi na ujenzi utaanza katika mwaka wa fedha 2023/2024 na kutekelezwa kwa kipindi cha miaka miwili. Kukamilika kwa miradi hiyo kutawezesha wakazi wa Mji Mlowo kupata huduma ya majisafi, salama na yenye kutosheleza.