Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. REHEMA J. MIGILLA aliuliza: - Je ni lini Serikali itaanza kutekeleza mradi wa ujenzi wa bwawa katika Kijiji cha Ichemba?

Supplementary Question 1

MHE. REHEMA J. MIGILLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nishukuru majibu ya Serikali. Bwawa hili la Chemba ni bwawa kubwa sana na likikamilika lina uwezo wa kwenda kuhudumia kata zangu tisa za Jimbo la Ulyankulu na bwawa hili lina maji mengi sana baada ya upembuzi yakinifu na tayari Serikali imeshatutengea milioni 750 kwa ajili ya ujenzi wa bwawa hili kwa ajili ya matumizi ya nyumbani. Sasa Je, upi ni mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba maji haya yataendelea kutumika pia kwenye shughuli za umwagiliaji?

Lakini swali lingine la pili, Je, Mheshimiwa Naibu Waziri upo tayari kuongozana na mimi ili Bunge linapokwisha hapa uende uone hali halisi ya bwawa hilo?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema katika majibu yangu ya msingi ya kwamba kwa kutambua kwamba tunalo bwawa kubwa ambalo ni chanzo kizuri cha maji kwenye kilimo cha umwagiliaji, Serikali itahakikisha kwamba katika mwaka wa fedha ujao tunafanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ili maji yale pia yatumike kama sehemu ya kilimo na yaguse eneo kubwa zaidi ya kata tisa za Ulyankulu ili wananchi waweze kunufaika na bwawa hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la pili niko tayari kuongozana na Mheshimiwa Mbunge kwenda jimboni kuangalia jambo hili pamoja na watalaam wetu ili kuweza kuharakisha zaidi ili wakulima wa Ulyankulu waanze kulima kupitia chanzo hiki cha maji kupitia mfumo wa umwagiliaji.

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. REHEMA J. MIGILLA aliuliza: - Je ni lini Serikali itaanza kutekeleza mradi wa ujenzi wa bwawa katika Kijiji cha Ichemba?

Supplementary Question 2

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuweza kuuliza swali la nyongeza. Je, Serikali ina mkakati gani wa kutumia bonde la Kiru na Magara kwa ajili ya umwagiliaji?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye kiambatanisho namba tano cha bajeti yetu tuliyoisoma hapa ndani tumeyataja mabonde 22 moja kati ya mabonde yaliyotajwa ni mabonde ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyataja na yapo katika hatua ya mshauri mwelekezi hivi sasa akikamilisha kazi tunaanza ujenzi mara moja ili wananchi wa Mkoa wa Manyara waweze kunufaika na skimu hizi za umwagiliaji.

Name

Nicholaus George Ngassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. REHEMA J. MIGILLA aliuliza: - Je ni lini Serikali itaanza kutekeleza mradi wa ujenzi wa bwawa katika Kijiji cha Ichemba?

Supplementary Question 3

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Jimbo la Igunga tuna skimu kubwa ya umwagailiaji ya Mamapuli iliyopo pale Mwanzugi na kwenye bajeti inayotembea, Serikali iliahidi kutupatia fedha. Je, ni lini Serikali itatupatia fedha kwa ajili ya kuboresha miundombinu ili kuboresha miundombinu kwa ajili ya kuwahudumia wakulima waliopo ndani na nje ya skimu? Ahsante.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, skimu hii ni kati ya skimu 42 ambazo tumezitengea fedha na nimtoe hofu tu Mheshimiwa Mbunge ya kwamba tutakamilisha yale ambayo tuliahidi ndani ya Bunge hili kuhakikisha kwamba skimu ile inafanya kazi na inarekebishwa ili wananchi waweze kufanya kilimo cha umwagiliaji kupitia skimu hiyo.