Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 48 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 634 2023-06-14

Name

Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. REHEMA J. MIGILLA aliuliza: -

Je ni lini Serikali itaanza kutekeleza mradi wa ujenzi wa bwawa katika Kijiji cha Ichemba?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo napenda kujibu swali la Mheshimiwa Rehema Juma Migilla, Mbunge wa Ulyankulu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi huu wa ujenzi wa bwawa ambao upo katika Kata ya Ichemba, Wilaya ya Kaliua unategemewa kukusanya maji ya matumizi ya nyumbani, pamoja na umwagiliaji kwenye mashamba na unategemewa kunufaisha wananchi wapatao 18,000 wa Kata ya Ichemba na maeneo mengine ya Ulyankulu. Zabuni ya kumpata mkandarasi kwa ajili ya ujenzi wa bwawa hilo imeshatangazwa na RUWASA na taratibu zingine zinaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika bajeti ya mwaka 2024/2025 Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji itatenga fedha kwa ajili ya upembuzi yakinifu, usanifu wa kina na ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji ambayo zitatoa maji kwenye bwawa na kupeleka mashambani.