Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Leonard Mtega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga minara ya simu maeneo yasiyo na mawasiliano hususan Kata za Ipwani, Miyombweni na Igava?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS L. MTEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Pia nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, hususan katika kata hizi tatu, lakini nina swali dogo la nyongeza: Je, Serikali iko tayari kupeleka mawasilino katika maeneo mengine yenye shida kama vile Ihahi, Azimio Mswiswi, Mapula, Ilaji, Igalako, Uhambule, Chamoto, Mbaliro na Matebete? Ahsante. (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Francis Leonard Mtega, Mbunge wa Jimbo la Mbarali, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kata ambazo Mheshimiwa Mbunge amezitaja zina mitandao isipokuwa jambo ambalo lipo kwa sasa ni kwamba, unakuta kata moja ina mtandao wa Halotel lakini wananchi wanahitaji Airtel, na kata nyingine wana Airtel lakini wananchi wanahitaji Vodacom.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote Na. 11 ya Mwaka 2006 lengo lake lilikuwa kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma ya mawasiliano, hata angalau kwa mnara mmoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia Sheria yetu ya EPOCA Na. 3 inampa Mheshimiwa Waziri mamlaka ya kutunga kanuni. Sasa ili tutatue changamoto ya kuwa na minara mingi ndani ya eneo moja na kuwa na utitiri ndani ya eneo moja, tumeamua sasa kuingia kwenye kanuni ambayo inaelekeza watoa huduma; cha kwanza tuwe na infrastructure sharing, maana yake tukiwa na mnara mmoja watoa huduma wote watakwenda kuweka huduma ya mawasiliano pale ili Watanzania wote waweze kupata huduma hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine tumeliongeza kuhakikisha kwamba tuna-share ile spectrum (masafa), badala ya kila mtoa huduma kuja na masafa yake, basi tumeruhusu ambapo sheria hapo kabla ilikuwa inazuia, sasa tumeruhusu ili kuhakikisha kwamba Waheshimiwa wote wenye changamoto za mawasiliano tuweze kuwapatia huduma kwa urahisi bila kuleta utitiri wa minara ndani ya nchi yetu, ahsante sana.

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga minara ya simu maeneo yasiyo na mawasiliano hususan Kata za Ipwani, Miyombweni na Igava?

Supplementary Question 2

MHE. DAVID M. KIHENZILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa. Iliwahi kuahidiwa hapa Bungeni juu ya kutupatia minara kwenye Kata za Maduma, Kitasengwa, Kasanga na Makungu na Kasanga kuna kituo cha afya: Je, lini Serikali itatimiza ahadi hii?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa David Kihenzile, ameshaleta changamoto hii na tunafahamu kwamba eneo la Kasanga kuna kituo cha afya, na ili kuhakikisha kwamba kituo kile kinafanya kazi kwa kutumia mifumo ya TEHAMA, ni lazima tufikishe huduma ya mawasiliano. Maeneo haya ya Maduma, Makungu pamoja na Kasanga tumeshaingiza kuhakikisha kwamba yanatekelezwa ili wananchi wa maeneo hayo wapate huduma ya mawasiliano, ahsante sana.

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga minara ya simu maeneo yasiyo na mawasiliano hususan Kata za Ipwani, Miyombweni na Igava?

Supplementary Question 3

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kata za Busale, Ibanda na Itope zipo mpakani sana mwa Malawi, na siku zote unapopita kwenye kata hizo mawasiliano yanapokwa na Wamalawi. Hata juzi Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya, Josephine Keenja, ameshuhudia hoteli zote zilizopo mpakani zilivyokosa wateja kwa kukosa mawasiliano: Je, ni lini sasa Serikali itatuondoa kwenye utumwa huo wa kubaki kama Wamalawi wakati sisi ni Watanzania?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ally Anyigulile Jumbe, Mbunge wa Jimbo la Kyela, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla ya kuwa na Mradi wa Tanzania ya Kidigitali, tulikuwa na mradi wa special zones and boarders. Mradi huu ulikuwa mahususi kwa maeneo ya mipakani, hasa kule ambapo kuna mwingiliano wa mawasiliano na nchi za jirani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunafahamu kwamba mawasiliano ni uchumi katika maeneo ya mpakani, tunafahamu mawasiliano ni usalama, lakini ni haki ya msingi ya kila Mtanzania kwa mujibu wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi, kuhakikisha kwamba wanapata mawasiliano. Kwa vile Mheshimiwa Mbunge amesema, basi tutatuma timu yetu tukajiridhishe tena kuona ni maeneo yapi ambayo yamebaki kuwa na changamoto hizo ili tuweze kuchukua hatua, ahsante sana.

Name

Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga minara ya simu maeneo yasiyo na mawasiliano hususan Kata za Ipwani, Miyombweni na Igava?

Supplementary Question 4

MHE. LUHAGA J. MPINA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa nafasi. Kwa kuwa Serikali katika Jimbo la Kisesa ilishaahidi kujenga mnara katika Kata za Isengwa, Mbugabanya, Mwabusalu, Mwakisandu, Lingeka na Mwabuma: Ni lini Serikali itatimiza azma yake hiyo ili kuboresha mawasiliano katika kata hizo? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Luhaga Joelson Mpina, Mbunge wa Jimbo la Kisesa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge alileta kata sita ambazo zilikuwa na changamoto, na kweli nasi tukajiridhisha kuna changamoto hiyo. Baada ya kupitia na kuangalia bajeti yetu, Mheshimiwa Rais ameridhia kupeleka fedha za ujenzi wa minara katika Kata za Mwabuma, Isengwa pamoja na Mwabusalu ambapo watoa huduma wa Airtel na TTCL watakwenda kujenga. Kata nyingine ambazo zimebaki, tunazipokea kama Serikali, fedha zitakapopatikana tutahakikisha kwamba tunafikisha huduma ya mawasiliano, ahsante sana.

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga minara ya simu maeneo yasiyo na mawasiliano hususan Kata za Ipwani, Miyombweni na Igava?

Supplementary Question 5

MHE. MASHIMBA M. NDAKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Kata za Mwabayanda, Kulimi na Kata ya Mwangonoli zote hazina kabisa mawasiliano ya simu. Je, Serikali ina mpango gani kuzipatia kata hizi mawasiliano ya simu?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mashimba Ndaki Mbunge wa Maswa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kata hizi ambazo Mheshimiwa Mbunge amezitaja, tumeziingiza kwenye awamu ya kufanya tathmini. Tumeshafanya awamu ya kwanza, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge baada ya kutoka hapa hizi kata kwa ustadi kabisa tuzipitie ili tukaziingize katika utaratibu wa kuzifanyia tathmini na pale fedha zitakapopatikana tuhakikishe tunafikisha huduma ya mawasiliano katika kata hizi, ahsante sana.

Name

Dr. Alice Karungi Kaijage

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga minara ya simu maeneo yasiyo na mawasiliano hususan Kata za Ipwani, Miyombweni na Igava?

Supplementary Question 6

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa tuna Mkongo wa Taifa. Sasa Serikali haioni kuna haja ya kufunga minara hii hasa pembezoni ili kupunguza mahangaiko ya watumishi wawe na utulivu huko pembezoni wafanye shughuli zao kule kule hata kama kusoma wasome online?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Alice Karungi Kaijage kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iliingia kwenye mpango wa kujenga Mkongo wa Taifa. Mkongo wa Taifa faida yake ni kwamba unaweza kupitisha traffic kwa wingi tena kwa kasi ya mwanga lakini vilevile lengo la kujenga Mkongo wa Taifa ni kuondokana na mifumo tuliyokuwa tunatumia zamani ya microwave lakini japo microwave kuna maeneo ambayo bado tunatumia. Lengo la kuwa na Mkongo wa Taifa ni kwamba baadae tutaunganisha minara ili kuhakikisha kwamba huduma inaweza kupatikana popote pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mambo makubwa ambayo tayari yameshafanyika, ambayo ni faida kubwa inayotokana na mkongo wa Taifa. Kwa sasa tuna vitu tunaita telecentre, telecentre hizi maana yake kuna maeneo ambapo mgonjwa haitaji kufika Muhimbili anaweza akapatiwa huduma akiwa Bukoba, akiwa Kagera, akiwa Mtwara lakini ile taarifa yake ikasomwa Muhimbili kule kwa sababu ya uwepo wa Mkongo wa Taifa wa mawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo tunaomba pia tupokee ushauri wako tutaendelea kuboresha kuhakikisha kwamba nchi yetu inazidi kuhakikisha kwamba mifumo yote na huduma zote zinatolewa kwa kidigitali kwani ndio msingi halisi wa uchumi wa sasa, ahsante sana.

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga minara ya simu maeneo yasiyo na mawasiliano hususan Kata za Ipwani, Miyombweni na Igava?

Supplementary Question 7

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Jimbo la Kalenga Kata za Masaka pamoja na Kianga zina changamoto ya mawasiliano kwa muda mrefu. Je, ni lini sasa Serikali itapeleka mawasiliano?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nipokee changamoto ya mawasiliano hayo ili tuweze kukaa na kuweza kuyapitia vizuri lakini naamini kwamba katika kata zake, Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Dkt. Samia Suluhu Hassan kuna minara tumempelekea katika jimbo lake na tunaamini kwamba kwa kiasi hicho kikubwa ni zaidi ya asilimia 70 ya upatikanaji wa huduma ya mawasiliano katika jimbo lake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini hizi kata ambazo amezitaja tunazipokea kwa ajili ya utekelezaji, ahsante sana.

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga minara ya simu maeneo yasiyo na mawasiliano hususan Kata za Ipwani, Miyombweni na Igava?

Supplementary Question 8

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, Makao makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Momba yako Chitete na kwa bahati mbaya eneo hili halijapitiwa na Mkongo wa Taifa hivyo kusababisha changamoto ya mawasiliano kwenye tarafa ya Kamsamba na tarafa yote ya Msangano. Je, ni lini tutachepushiwa Mkongo wa Taifa kwenye Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Momba?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Condester Michael Sichalwe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna njia tatu za kufikisha mawasiliano pale ambapo hatujafikisha Mkongo wa Taifa. Tunatumia microwave na pale ambapo microwave haiwezi kufikisha tunatumia Virtual Satellite lakini kwa sababu ni nia na dhamira ya Serikali kuhakikisha nchi yetu yote inafikiwa na Mkongo wa Taifa. Mpaka sasa tumeshafikia Mikoa 25 lakini baada ya kufika Mikoa 25 tutaenda sasa Wilaya kwa Wilaya na mpaka sasa tumeshajenga kilometa 8319 lakini vilevile katika bajeti ya miaka miwili iliyopitishwa na Bunge lako Tukufu. Mheshimiwa Rais aliridhia fedha takribani bilioni 345 kwa ajili ya kufikisha Mkongo wa Taifa katika maeneo mbalimbali ambapo ni kilometa 4442 zinaenda kujengwa nchi nzima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunaamini kwamba zikisha kamilika tutakuwa tumefikisha kilometa 12314 ambapo ni sawasawa na asilimia 85 ya utekelezaji na lengo la Ilani ya Chama cha Mapinduzi kufikia mwaka 2025, nakushukuru.