Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya kutoka Kibada – Tundwi hadi Songani kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa, barabara hiyo ya Kibada hadi Tundwi - Songani inakwenda mpaka Pemba Mnazi ambapo kuna viwanja vingi vimetengwa na Serikali, lakini kuna changamoto kubwa ya ukosefu wa Barabara. Ukosefu wa kujengwa barabara hiyo unasababisha kuongezeka kwa nauli kwa wananchi wa Kisarawe II, Mwasongwa na Tundwi - Songani.

Je, nataka commitment ya Serikali, ni lini? Je, ni kweli itaanza kujengwa barabara hiyo mwezi Juni, maana imekuwa ni ahadi ya muda mrefu.

Swali la pili, changamoto ya ukosefu wa barabara inaikumba pia Halmashauri ya Ubungo. Barabara ya Victoria – Mbezi – kwa Yusufu hadi Mpiji Magohe. Ni lini barabara hiyo nayo itajengwa?(Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na swali la kwanza la Mheshimiwa Mariam Nassoro Kisangi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba, barabara hii niliyoitaja tunakwenda kuijenga, ndiyo maana bila kusita tunategemea mwezi kabla haujaisha huu wa Juni tuwe tumeisaini kwani Mkandarasi alishapatikana tuanze ujenzi wa barabara hii. Tunatambua umuhimu wa barabara hii kwani sasa limekuwa ni eneo muhimu sana kwa shughuli za kiuchumi kwa wananchi wa Dar-es-Salaam na hasa Jimbo la Kigamboni. Pia ni kwamba, tunajua alikuwa amepata changamoto ya kuharibika, Mkandarasi tayari yupo site kuanzia Mji Mwema, Kimbiji lakini Mji Mwema - Mwasonga hadi Kimbiji kuhakikisha kwamba, anarudisha barabara kwenye hali yake nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu barabara alizozitaja hizi tayari, kama ataangalia kwenye bajeti za Jimbo la Ubungo, barabara hizi tumeziingiza kwenye mpango. Kulikuwa na barabara moja ilikuwa haijafanyiwa usanifu hasa ile ya Kwa Yusufu - Makabe, lakini barabara nyingine hizi tumeziweka kwenye mpango wa kuanza kuzijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya kutoka Kibada – Tundwi hadi Songani kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Barabara ya Mbuyu wa Mjerumani – Magara – Mbulu ni muhimu sana inayounganisha Mkoa wa Manyara na Wilaya za Mbulu na Mji wa Arusha: Je, kwa nini Serikali imeshimdwa kutekeleza eneo la mlima Magara ambalo lina jiografia ngumu sana na inatumia gharama kubwa kwa kiwango cha changarawe? Lini itaweka lami mlima Magara?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Barabara ya Mbuyu wa Mjerumani – Magara hadi Mbulu ni barabara ambayo inapita kwenye escarpment. Mheshimiwa Mbunge atakuwa ni shahidi kwamba tunachokifanya sasa hivi, ni kukamilisha eneo lote la ule mwinuko kujenga kwa kiwango cha lami au kiwango cha zege. Baada ya kukamilisha hayo maeneo ambayo yamekuwa ni changamoto kubwa, mpango sasa ni kuijenga barabara yote kwa kiwango cha lami, kwani usanifu tayari umeshafanyika, ahsante.

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya kutoka Kibada – Tundwi hadi Songani kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika jibu la msingi katika swali hili ambalo limetoka kwa Mheshimiwa Mariam Kisangi, umesema kwamba barabara ile inakwenda kujengwa kwa kiwango cha lami, tunashukuru kwa hilo, lakini barabara hii kwa sasa hivi imeharibika sana kutokana na uzito wa magari yanayopita pale pamoja na mvua ambazo zimenyesha: Ni lini ukarabati wa barabara hii utafanyika wakati tunasubiri barabara hii kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Faustine Engelbert Ndugulile, Mbunge wa Kigamboni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara nyingi za Dar es Salaam, hasa ambazo ni kwa kiwango cha changarawe, zimepata changamoto kutokana na mvua ambazo zimekuwa zinaendelea kunyesha katika Mkoa wa Dar es Salaam, lakini nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika barabara zake hizo alizozitaja, tayari tumesham-engage Mkandarasi, Ibra Construction Company ambaye amepewa barabara ya kutoka Mji Mwema kwenda Kimbiji na pia huyu huyo atafanya kazi kutoka Kibada – Mwasonga – Kimbiji na kuendelea mbele ili kurejesha mawasiliano na kuondoa changamoto ambazo zinaendelea kwa sasa. Kwa hiyo, mkandarasi tayari ameshakuwa site, ahsante.

Name

Twaha Ally Mpembenwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya kutoka Kibada – Tundwi hadi Songani kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Jimbo la Kibiti wamenituma niulize kwa mara nyingine tena, ni nini mpango au mkakati wa Serikali kuhusiana na barabara ya Kibiti – Dimani mpaka Mloka?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Twaha Ally Mpembenwe, Mbunge wa Kibiti, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii sasa hivi tunairudisha tena kuifanyia review ya usanifu, lakini naamini ndiyo barabara ambayo tayari tunajenga lile Daraja kubwa la Mbambe kuhakikisha kwamba tunaondoa hiyo changamoto. Mpango ni kuijenga hiyo barabara kwa kiwango cha lami, ambayo pia ni barabara fupi sana kwenda Bwawa la Nyerere ukitokea Pwani, ahsante.

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya kutoka Kibada – Tundwi hadi Songani kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. DAVID M. DAVID: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Barabara ya milimani ya Vudee ni fupi sana, lakini kila mwaka Serikali inamwaga kifusi na mvua inaponyesha, basi inazolewa na maji: Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari sasa kwamba tukimaliza Bunge twende Vudee milimani ili akaone barabara hii inayokwenda mpaka Ndolwa ili iweze kutengenezwa kwa kiwango cha lami au zege ili Serikali isipoteze fedha?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubalina na Mheshimiwa Mbunge kwamba maeneo ya milimani kwa kweli yana changamoto kubwa. Kwanza nitoe maelekezo kwa Meneja wa TANROADS Mkoa wa Kilimanjaro aitembelee hiyo barabara. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, baada ya Bunge twende tukaipitie, lakini twende wakati mtaalam ameshapita ili tuwe tayari tuna taarifa za awali kuhusu changamoto ambazo ziko kwenye hiyo barabara. Kwa hiyo nakubali, tutakwenda kuitembelea hiyo barabara, ahsante.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya kutoka Kibada – Tundwi hadi Songani kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 6

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Watu wa Tarime wanamshukuru sana Mheshimiwa Rais, Mama wa Taifa, kwa kutoa fedha ya kujenga lami kilometa 25. Sasa naomba nijue: Lini kipande cha kitoka Kwinogo – Nyamongo hadi Serengeti Mugumu kitaanza kujengwa kwa kiwango cha lami? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, tulishaongea na Mheshimiwa Mbunge, na kweli kipande hicho tutakijenga kwa kiwango cha lami. Tayari mkandarasi alishapatikana, taratibu za manunuzi zimeshapatikana. Tunachofanya sasa katika maandalizi ni kutafuta siku ya kusaini kipande kilichobaki cha kutoka Nyamwaga hadi Mugumu - Serengeti kwa kiwango cha lami.

Name

Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya kutoka Kibada – Tundwi hadi Songani kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 7

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Swali hili hili ambalo limeulizwa na Mheshimiwa Mbunge wa Tarime Vijijini, nimeuliza mara nyingi na ni mara nyingi nimeongea na Mheshimiwa Naibu Waziri kuhusu barabara hii ya Nyamongo mpaka Mugumu: Sasa tunaomba kujua ni lini hasa kwa maana ya tarehe, utakaposainiwa huo mkataba na kuanza ujenzi wa barabara ya Nyamongo – Mugumu?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jeremiah Mrimi Amsabi, Mbunge wa Serengeti, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, labda tu niwafahamishe Waheshimiwa Wabunge, na hasa Mbunge wa Tarime na Mbunge wa Serengeti, hii barabara inaunganisha Serengeti na Tarime, lakini kutoka Serengeti pia inategemea kwenda Nata. Naomba wawe na Subira. Taratibu zote za manunuzi zimeshakamilika, tunachosubiri ni kutafuta siku maalum ya kufanya signing.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tuna hakika, kama utaratibu utakwenda kama tulivyopanga ni kuisaini hiyo barabara kabla ya mwisho wa mwaka huu wa fedha. Kwa hiyo, siku itakapokuwa tayari, tutawajulisha Waheshimiwa Wabunge, Mheshimiwa Mbunge wa Serengeti na Mheshimiwa Mbunge wa Tarime Vijijini, ahsante.

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya kutoka Kibada – Tundwi hadi Songani kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 8

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukifika Chalinze kuna roundabout nzuri kuliko roundabout yoyote hapa nchini, lakini pale kuna kilometa 25 kufika Magindu: Ni lini barabara ile itajengwa kwa kiwnago cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hawa Mchafu Chakoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tushukuru kwamba keep left ile ni kati ya keep left nzuri katika nchi yetu. Hiyo barabara aliyoitaja ya Chalinze – Magindu katika bajeti inayokuja imepangwa ifanyiwe usanifu yakiwa ni maandalizi ya kuijenga hiyo barabara kwa kiwango cha lami.

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya kutoka Kibada – Tundwi hadi Songani kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 9

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Sisi tuna barabara ya kutoka Namtumbo – Mtonya – Mgombasi, kuna daraja katika Mto Luwegu ambalo linahatarisha maisha ya watu, kwani ni jembamba sana: Je, Serikali inaweza kuiwekea fedha kulijenga daraja hilo ili kuepusha maafa yanayoweza kutokea? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwanza nipokee ombi la Mheshimiwa Mbunge kwa sababu daraja hilo linahatarisha maisha ya wananchi. Pia nimwelekeze Meneja wa TANROADS Mkoa wa Ruvuma ili aiangalie hiyo barabara kwa maana ya Namtumbo – Mto Luwegu hadi Mgombasi, pia akaangalie daraja hilo, afanye tathmini, halafu alete Makao Makuu kwa ajili ya kutafuta fedha kulijenga hilo daraja la Mto Luwegu, ahsante.

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya kutoka Kibada – Tundwi hadi Songani kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 10

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa Serikali imejenga madaraja mazuri kwenye barabara ya Lupila kwenda Ikonda: Je, lini mtajenga kwa kiwango cha lami ili kukamilisha kazi ile nzuri na wananchi wetu wakaweza kupita vizuri kwenye barabara ile? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Neema Mgaya, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, azma ya Serikali ni kujenga hizi barabara kwa kiwango cha lami. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwa kuwa tumeshaanza kujenga hii barabara nzuri, tutahakikisha tunaifikisha mwisho ikiwa ni pamoja na barabara aliyoitaja kuijenga kwa kiwango cha lami kulingana na upatikanaji wa fedha, ahsante.

Name

Prof. Kitila Alexander Mkumbo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ubungo

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya kutoka Kibada – Tundwi hadi Songani kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 11

MHE. PROF KITILA A. MKUMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Barabara ya Kimara – Mavurunza mpaka Segerea imewekwa kwenye bajeti ya mwaka huu, lakini kwa sasa haipitiki, hali yake ni mbaya sana: Kwa nini Serikali isifanye matengenezo wakati tukisubiri ujenzi wa lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Prof. Kitila Alexander Mkumbo, Mbunge wa Ubungo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema, barabara za Dar es Salaam nyingi ambazo siyo kwa kiwango cha lami ziko kwenye mazingira magumu. Nimwagize Meneja wa TANROADS Mkoa wa Dar es Salaam, aende kwenye barabara hii ambayo inaunganisha Jimbo la Mheshimiwa Prof. Kitila Mkumbo na Mheshmiwa Bonnah, waende wakaiangalie ili waweze kuondoa hizo changamoto na waweze kurejesha usafiri kati ya hayo majimbo mawili, ahsante.

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya kutoka Kibada – Tundwi hadi Songani kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 12

MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi. Serikali ya Awamu ya Tano iliahidi kuwajengea wananchi wa Minziro barabara ya kutoka Mutukula kwenda mpaka Minziro, na ni faraja kwamba Naibu Waziri alikuja akatembelea barabara hiyo na sasa hivi imeanza kufumuliwa: Je, lini sasa barabara hiyo itakamilika kwa kiwango cha lami kutoka Mutukula kwenda Minziro?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, barabara hii tulitembea na Mheshimiwa Mbunge, mimi nilishaitembelea. Kitu cha kwanza kilikuwa ni kuifungua hiyo barabara, na kitu cha pili tutakachofanya sasa ni kuifanyia usanifu. Ni barabara muhimu kwa sababu ipo kwenye uchumi na pia ni barabara ya ulinzi ambayo ni moja ya vipaumbele vya kujenga barabara kwa kiwango cha lami kwa mujibu wa sera zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimhakikishe Mheshimiwa Mbunge kwamba baada ya kuifungua yote tutaifanyia usanifu ikiwa ni maandalizi ya kuijenga kwa kiwango cha lami, ahsante.