Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 48 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 632 2023-06-14

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya kutoka Kibada – Tundwi hadi Songani kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nipokee marekebisho ya Mheshimiwa Mbunge aliyoyasema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mariam Nassoro Kisangi, Mbunge Viti Maalum, Mkoa wa Dar-es-Salaam, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imepanga kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Kibada – Tundwi, Songani, Kimbiji yenye urefu wa kilometa 41 ambapo kwa sasa upo kwenye hatua za mwisho za manunuzi ya kumpata Makandarasi atakayetekeleza ujenzi wa mradi huu. Mkataba unatarajiwa kuwa umesainiwa kabla ya mwisho wa mwezi huu Juni, 2023. Ahsante.