Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza:- Je, lini ujenzi wa barabara ya njia nne kuanzia Tengeru utaendelea ikiwa ni mwendelezo wa barabara ya Sakina – Holili?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa barabara za lami huwa unaboresha sana mazingira na mandhari ya nchi yetu kule inakopita. Barabara hii pale inapoanzia kuna soko la Tengeru ambalo hali yake ni mbaya kimazingira na miundombinu, lakini tunajua kwamba, miradi mikubwa hii ina-component ya CSR.

Je, Serikali ina mpango gani wa kusaidia Halmashauri ya Meru kuboresha soko hili kwa kutumia CSR yake?

Swali la pili, kwa kuwa, mradi huu uko kwenye hatua ya usanifu na upembuzi yakinifu, Serikali haioni ni busara kuweka uboreshaji wa soko hili katika usanifu huo? Nakushukuru. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili kwa pamoja ya Mheshimiwa Dkt. John Danielson Pallangyo, Mbunge wa Arumeru, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwenye miradi hii mikubwa kunakuwa na component ya CSR. Ninachoweza kumuomba Mheshimiwa Mbunge, tumelipokea ombi lake la kuboresha hiyo miundombinu ya soko la Tengeru pamoja na barabara inayoingia, lakini tu pengine nishauri ni vyema tukapata maombi rasmi ili tuweze kuyaratibu kabla Mhandisi Mshauri hajakamilisha, basi iwe ni sehemu ya mpango wa kuijenga hiyo barabara ikiwa ni pamoja na kujenga hiyo barabara ndogo ya kuingia kwenye soko na kuboresha hilo soko, ahsante. (Makofi)

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza:- Je, lini ujenzi wa barabara ya njia nne kuanzia Tengeru utaendelea ikiwa ni mwendelezo wa barabara ya Sakina – Holili?

Supplementary Question 2

MHE. NUSRAT S. HANJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini sasa Serikali itajenga barabara ya Singida – Sepuka – Ndago kwa kiwango cha lami ambayo kimsingi ni barabara muhimu sana kwa wananchi na wakazi wa Tarafa ya Sepuka, Jimbo la Singida Mashariki?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara aliyoitaja ya Singida – Sepuka – hadi Ndago ni barabara ambayo tunategemea muda wowote kusaini mkataba kwa ajili ya kuanza ujenzi kwani tayari taratibu zote za manunuzi zimeshakamilika. Kwa hiyo, kinachosubiriwa tu ni kuisaini ili ujenzi uanze kujenga barabara hiyo yote kwa kiwango cha lami. Ahsante.(Makofi)

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza:- Je, lini ujenzi wa barabara ya njia nne kuanzia Tengeru utaendelea ikiwa ni mwendelezo wa barabara ya Sakina – Holili?

Supplementary Question 3

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni lini barabara nne zitajengwa eneo la Nyangole, Bukoba Mjini ili kutimiza ahadi ya Makamu wa Rais?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara nne eneo la Nyangole, ambayo iko Bukoba Mjini ilikuwa ni ombi la Mheshimiwa Mbunge wa Bukoba Mjini, Mheshimiwa Byabato, wakati Makamu wa Rais amefanya ziara katika Mji wa Bukoba. Ninamshukuru kwanza Mheshimiwa Oliver Semuguruka, Mbunge, kwa kuendelea kufuatilia utekelezaji wa ahadi hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge Oliver pamoja na Mheshimiwa wa Bukoba Mjini na wananchi wa Bukoba Mjini agizo hilo tayari tumeshaanza utekelezaji. Katika hii barabara tutafanya kazi tatu, moja itakuwa ni kuondoa, kupunguza zile kona, kupunguza mteremko, lakini pia kujenga barabara ya njia mbili zinazoshuka na njia mbili zinazopanda, tutaanza na kilometa nne, lakini mpango ni kujenga kilometa tano kutoka hapo Nyangoya hadi Bukoba bandarini. Ahsante. (Makofi)