Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 48 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 631 2023-06-14

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza:-

Je, lini ujenzi wa barabara ya njia nne kuanzia Tengeru utaendelea ikiwa ni mwendelezo wa barabara ya Sakina – Holili?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. John Danielson Pallangyo, Mbunge wa Arumeru Mashariki, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imepanga kuendeleza ujenzi wa barabara ya njia nne kuanzia Tengeru kwa kutumia fedha za mkopo nafuu kutoka Shirika la Maendeleao la Japan (JICA). Ujenzi utahusisha sehemu ya barabara ya Tengeru – Usa River yenye urefu wa kilometa 9.3, sehemu ya Moshi Mjini yenye urefu wa kilometa 8.4 na ujenzi wa daraja jipya la Kikafu lenye urefu wa mita 360. Kwa sasa mchakato wa manunuzi ya kumpata Mhandisi Mshauri kwa ajili ya kufanya kazi ya usanifu wa kina wa barabara na daraja upo katika hatua za mwisho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kukamilika kwa usanifu, kazi ya ujenzi itaanza. Ahsante.