Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa fedha ili kukamilisha ujenzi wa Kituo cha Polisi Wilayani Kishapu?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninaipongeza Serikali kwa jitihada hizi ambazo imeweka mipango ya kuhakikisha kwamba, mwaka 2023/2024 ujenzi huu unakamilika.

Swali langu la kwanza, Mheshimiwa Naibu Waziri uko tayari kuambatana na mimi ili kwenda kuona jitihada zilizofanywa na Mfuko wa Jimbo wa kwangu kama Mbunge, lakini nguvu za wananchi, wadau wa maendeleo kama Mgodi wa Mwadui Williamson?

Swali la pili, Mheshimiwa Waziri, utakuwa tayari pia kwenda kuona jitihada kubwa zinazofanyika za kupata eneo katika Mji Mdogo wa Maganzo, ili tuweze kujenga kituo kingine kwa sababu Kituo kile cha Maganzo ni chakavu na bado kinahudumia Kata tano, Kata ya Mwadui Luhumbo, Kata ya Mondo, Kata ya Songwa na Kata ya Maganzo yenyewe ili kwamba, tuone namna ya kuweza kuwapa huduma kwa usahihi na katika hali ya ubora wananchi wanaozunguka maeneo hayo?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tumpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa juhudi anazofanya na wadau walioko Kishapu katika ujenzi wa vituo vya Polisi kwa ajili ya usalama wa mali za wananchi na wananchi wenyewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu utayari wangu kuongozana nae, Mheshimiwa nimeshakuahidi na hapa ninathibitisha kwamba, baada ya kumaliza Bunge letu hili mwezi Julai nitakuwa tayari kwenda Kishapu, pamoja na mambo mengine, kuona jitihada za wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini njambo la pili, tunatambua kweli katika Mji Mdogo wa Maganzo kuna shughuli nyingi za kibiashara na huko kwenye Mgodi muhimu wa Mwadui wa madini ya Almasi. Tunatambua uchakavu wa kituo kilichopo na kwamba kimebanwa sana na wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo ambalo naweza nikashauri mapema kabla sijaja huko, ni kupata eneo ili tukiona kwamba eneo hilo linatosha tuliingize kwenye mpango wetu wa kujenga kituo kinachostahili kwenye eneo hilo la Maganzo. Nashukuru.

Name

Zuena Athumani Bushiri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa fedha ili kukamilisha ujenzi wa Kituo cha Polisi Wilayani Kishapu?

Supplementary Question 2

MHE. ZUENA A. BUSHIRI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha Polisi Siha?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo nimekuwa nikijibu hapa, kwa maeneo ambayo tumeona jitihada za Halmashauri na wananchi katika ujenzi wa vituo vya polisi ni kipaumbele cha Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi pamoja na Jeshi la Polisi kuwaunga mkono ili kukamilisha. Tutaangalia katika mipangilio yetu namna ambavyo tunaweza tukapata fedha kupitia ama vyanzo vya fedha za maendeleo kutoka Serikali Kuu au fedha za tuzo na tozo kuwaunga mkono wananchi wa Siha kukamilisha kituo chao cha Polisi, nashukuru.

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa fedha ili kukamilisha ujenzi wa Kituo cha Polisi Wilayani Kishapu?

Supplementary Question 3

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Kata ya Goba, Mtaa wa Tegeta A wameweka nguvu zao nyingi sana kujenga Kituo Polisi chenye hadhi ya ghorofa moja kuungana na nguvu za Mbunge Mfuko wa Jimbo. Je, Mheshimiwa Waziri utakuwa tayari kuja Kibamba kuona ile kazi kubwa iliyofanywa na wananchi wale wa Tegeta A juu ya ukamilishaji wa kituo hicho?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, niko tayari. Kwa juhudi zinazofanywa na Mheshimiwa Mtemvu na wananchi wake na wadau wengine katika jimbo lake niko tayari kwenda kushuhudia jitihada hizo na kuelekeza kuwaunga mkono kutoka Jeshi la Polisi ili kukamilisha vituo ambavyo tayari wameshavianzisha kwenye Jimbo lake, nashukuru.

Name

Martha Festo Mariki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa fedha ili kukamilisha ujenzi wa Kituo cha Polisi Wilayani Kishapu?

Supplementary Question 4

MHE. MARTHA F. MARIKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipatia nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Tanganyika hatuna kabisa Kituo cha Polisi, lakini wananchi wa Wilaya hiyo wameonesha juhudi kwa kuanzisha ujenzi wa kituo cha polisi kwa kujenga msingi. Je, ni lini Serikali itaunga juhudi hizo kwa kutupatia pesa ili tuweze kukamilisha kituo hicho?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuahidi Mheshimiwa Mariki kwamba, tunatambua umuhimu wa kuwa na Kituo cha Polisi chenye hadhi ya Wilaya na vituo vingine kwenye Tarafa husika katika Wilaya ya Tanganyika. Nimuahidi tu Mheshimiwa Mbunge, tumeshaongea hata na Mbunge wa Jimbo kwamba, kwenye bajeti yetu ijayo tutaona uwezekano wa kuwachangia ili waweze kujenga kituo hicho, tumuombe Mwenyezi Mungu liwezekane liweze kutekelezwa, nashukuru.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa fedha ili kukamilisha ujenzi wa Kituo cha Polisi Wilayani Kishapu?

Supplementary Question 5

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Mheshimiwa Waziri utakuwa tayari baada ya Bunge hili kufanya ziara kuja kuangalia nguvu za wananchi na Mbunge katika ujenzi wa Kituo cha Polisi kwenye Kata ya Nyijundu, Wilayani Nyang’hwale?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamuahidi nikitoka Shinyanga kwenda Nyag’hwale ni karibu sana, kwa hiyo, wakati namaliza ziara yangu Shinyanga pale Kishapu, kituo kitakachofuata ni Nyag’hwale ili kuona juhudi za wananchi hatimaye tumuunge mkono Mheshimiwa Mbunge. Nashukuru sana.