Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 48 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 630 2023-06-14

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa fedha ili kukamilisha ujenzi wa Kituo cha Polisi Wilayani Kishapu?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Boniphace Nyangindu Butondo, Mbunge wa Kishapu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo cha Polisi Wilaya ya Kishapu ni kituo cha Daraja B, na ujenzi wake umesimama ukiwa umefikia kwenye hatua ya umaliziaji. Tathmini kwa ajili ya kumalizia ujenzi imefanyika na kiasi cha shilingi 262,672,520 zinahitajika. Fedha hizo zimepangwa kutolewa kwenye mfuko wa tuzo na tozo katika mwaka wa fedha 2023/2024. Fedha zitakapotolewa ujenzi huo utakamilishwa, ili wananchi wa Kishapu waanze kunufaika na huduma za Polisi kupitia kituo hicho. Nakushukuru.