Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUM DAU HAJI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawezesha na kuwainua kiuchumi wanawake wasiojiweza?

Supplementary Question 1

MHE. MWANTUMU DAU. HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante. Nimshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake ya Serikali aliyoyatoa. Nina maswali yangu mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa kilimo BBT kwa vijana, Serikali ina mpngo gani wa kuja na BBT kwa wanawake wasiyosijiweza? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili je, Serikali haina umuhimu wa kuhakikisha mikopo hii inawafikia wanawake hao? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mwenyekiti, nakushukuru. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwantumu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli moja ya changamoto tulizonazo ni kuona namna gani ya kuwawezesha wanawake wawe na kesho nzuri kama ambavyo kuna programu hii ya kesho nzuri kwa vijana kwenye sekta ya kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani hili ni wazo zuri ili kuona namna gani tunawasaidia wanawake ambao ndio wana mchango mkubwa sana katika uchumi wa nchi hii. Nadhani kama Serikali tunachukua hili ili tuweze kuja na programu maalum yenye mlengo huo kwa ajili ya kuhakikisha wanawake wanakuwa na kesho nzuri kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la pili, ni dhahiri kweli Serikali tumeshaona changamoto zilizojitokeza kwenye mifuko mbalimbali ikiwemo ile 10% ilikuwa inatengwa na Halmashauri kwamba ilikuwa haiwafikii walengwa wakiwemo wanawake kutokupata kwa wakati na mambo mengine mengi. Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshatoa maelekezo tupitie upya namna ya kuhakikisha mifuko hii inawasaidia na hasa wanawake waweze kupata fedha zile kwa wakati, lakini kulingana na mahitaji yao. Sasa tunaangalia kwa namna ya pekee zaidi wanawake wasiojiweza ili waweze kupata mikopo au uwezeshaji huu kwa wakati kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge ameshauri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. MWANTUM DAU HAJI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawezesha na kuwainua kiuchumi wanawake wasiojiweza?

Supplementary Question 2

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Je, Serikali imefanya tathmini kujua kama majukwaa ya wanawake yanaleta tija katika wilaya zetu?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Komanya, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, majukwaa haya ya wanawake katika mikoa yamekuwa na tija kubwa, kwa sababu ndio ambayo yamepelekea wanawake wengi kupata mikopo, lakini pia kuwa na elimu ya ujasiriamali katika maeneo tofauti tofauti. Changamoto tuliyonayo ni kuona sasa tunawezesha zaidi majukwaa haya ya wanawake ili kuweza kupata mikopo kwa wakati, lakini yenye kutosheleza mahitaji yao kadri ambavyo wanaomba. Kwa hiyo kuna tathmini ya kutosha ambayo tunaifanya ili kuona namna gani zaidi ya kuendeleza majukwaa haya ya wanawake katika mikoa.

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUM DAU HAJI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawezesha na kuwainua kiuchumi wanawake wasiojiweza?

Supplementary Question 3

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kuuliza swali moja la nyongeza ambalo linasema hivi, kwa wale wanawake wanaofanya kazi maofisini, lakini kipato chao kidogo. Je, mnawawezesha vipi katika na wao kufanikisha masuala yao ya kuweza kujinyanyua kiuchumi? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Ni kweli, kuna wanawake ambao wanafanya kazi maofisi lakini mishahara yao kidogo haitoshi na hii ni kwa watumishi walio wengi, Serikali na hata katika sekta binafsi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna programu mahususi na Serikali wanafanya kwa wakati fulani kuhakikisha wanawapa upendeleo maalum kuwakopesha wakati mwingine mikopo ambayo haina riba. Pia kupitia ajira hizi watumishi hawa huwa wanapata kipaumbele kukopa katika taasisi za fedha, lakini pia wanaanzisha vikundi au SACCOS ambazo zenyewe zinawasaidia kujiwezesha kiuchumi au kupata fedha za ziada kwa wanawake ambao wanakuwa hawana uwezo au ambao mishahara yao ni kidogo katika maofisi yetu.

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUM DAU HAJI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawezesha na kuwainua kiuchumi wanawake wasiojiweza?

Supplementary Question 4

MHE. MINZA S. MJIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Napenda kujua Serikali inawasaidiaje wanawake wa Mkoa wa Simiyu ambao hawajiwezi kiuchumi na ambao hawapo kwenye mpango wa TASAF?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Ni kweli, katika mikoa au majimbo mengi ikiwemo Simiyu kuna wanawake wengi ambao hawana uwezo, hawajiwezi, lakini hawako kwenye ule mpango wetu wa TASAF. Moja ya maeneo ambayo tunayaangalia sasa kama nilivyosema ni kupitia zile 10% ambazo tunaweza kuzifanyia kazi na kuunganisha baadhi ya mifuko ambayo ilikuwa haiwafikii walengwa, ili tuone hawa ambao hawako kwenye TASAF lakini wana uhitaji maalum kama swali la msingi ulilouliza waweze nao kunufaika na fedha hizi za Mifuko ambayo itawasaidia kuweza kuanzisha shughuli mbalimbali za kijasiriamali, lakini pia kuinuka kiuchumi katika shughuli zao za kila siku.

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUM DAU HAJI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawezesha na kuwainua kiuchumi wanawake wasiojiweza?

Supplementary Question 5

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri. Kwa kujua kwamba Wilaya ya Same ina madini mengi ya gypsum hasa kwenye Kata za Bendera na Makanya na kwa kujua kwamba gypsum inaweza kuwa na products nyingi ambazo zitatengeneza ajira kubwa katika viwanda hivyo. Je, Serikali ina mpango gani wa kusaidia wananchi wa Wilaya ya Same kupata wawekezaji ili waweze ku-process ile gypsum wa-add value? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Naghenjwa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli moja ya maeneo ambayo tunayaangalia ni kuhamsisha uwekezaji katika sekta nyingi ikiwemo hii ya madini na hasa ya gypsum ambayo inatumika katika maeneo mengi kwenye ujenzi na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wanawake najua ndio wanashiriki sana katika shughuli za kiuchumi kama nilivyosema tutaona namna ya kukaa na Mheshimiwa Mbunge ili tuone kama kunakuwa na andiko kwa ajili ya Wilaya ya Same ambayo litavutia mahususi uwekezaji wa viwanda katika sekta hii kwa maana ya kuzalisha gypsum na shughuli nyingine za kiuchumi au viwanda vingine katika Jimbo la Same.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. MWANTUM DAU HAJI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawezesha na kuwainua kiuchumi wanawake wasiojiweza?

Supplementary Question 6

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri, je, SIDO imepotelea wapi kwa sababu kwenye Jimbo letu sijawahi kusikia SIDO, iko wapi?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Naomba nijibu swali la Dkt. Kimei, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, SIDO bado ipo na inaendelea kufanya shughuli zake, changamoto tuliyonayo ni mtaji mdogo wa kuweza kutoa huduma kama ilivyokusudiwa na shirika letu la kuendeleza viwanda vidogo na biashara ndogo Tanzania. Sasa tutakuja na sheria mahususi ili tuone namna gani ya kuiwezesha SIDO iweze kufanya shughuli zake kibiashara badala ya kutoa huduma ambayo inahitaji mtaji zaidi wa Serikali. Kwa hiyo tunadhani huu utakuwa ndio ufumbuzi ili waweze kuendesha shughuli zao kibiashara ili kuwafikia wajasiriamali wengi na wenye viwanda wengi zaidi kadri ambavyo uchumi wa sasa unataka.

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. MWANTUM DAU HAJI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawezesha na kuwainua kiuchumi wanawake wasiojiweza?

Supplementary Question 7

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa nafasi. Wilaya ya Chemba ni Wilaya ambayo ina maeneo mazuri na ya kutosha kwa ajili ya uwekezaji, lakini bahati nzuri sana tupo katikati ya Barabara ya c2c. Wizara ya Uwekezaji ina mpango gani wa kuwekeza kwenye Wilaya ya Chemba ambayo iko karibu kabisa na Makao Makuu ya Nchi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Mheshimiwa Monni ni kweli Chemba ni sehemu ya kimkakati kwa sababu iko katika barabara Kuu tunasema South – North Corridor ambayo tunaamini sasa kwa kufungua njia hizi kutakuwa na fursa nyingi za uwekezaji katika maeneo ya Chemba kama ilivyo Dodoma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie kwamba Serikali inaendelea kufanya jitihada za kuwatafuta wawekezaji, lakini nitumie fursa hii kumwomba Mheshimiwa Mbunge kushirikiana na halmashauri kuanza kutenga maeneo mahususi kwa ajili ya uwekezaji ili tunapopata wawekezaji wasipate kikwazo kwa maana ya kupata ardhi ambayo iko tayari kwa ajili ya uwekezaji katika sekta mbalimbali katika Jimbo la Mbunge.