Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 48 Investment and Empowerment Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 626 2023-06-14

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUM DAU HAJI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawezesha na kuwainua kiuchumi wanawake wasiojiweza?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakusukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mwantumu Dau Haji, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeanzisha mifuko na programu za uwezeshaji kwa lengo la kuwawezesha na kuwainua wananchi kiuchumi wakiwemo wanawake wasiojiweza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) imeendelea kutekeleza Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini - Awamu ya Pili kwa kuhawilisha ruzuku ili kuwawezesha wananchi wasiojiweza ikiwemo wanawake kupata mahitaji ya msingi ikiwa ni pamoja na kuwawezesha kujiunga kwenye vikundi na kuanzisha shughuli za kiuchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kutumia fursa hii kuwahimiza wanawake wasiojiweza kutumia fursa za uwepo wa mifuko na programu za uwezeshaji ili kuanzisha na kuendeleza biashara zao, nakushukuru sana.