Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA K.n.y. MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza siku za likizo kwa wazazi wanaojifungua watoto njiti?

Supplementary Question 1

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti nashukuru kwa nafasi hii nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, sasa Serikali haioni kwamba kuna haja ya kubadilisha sheria iliyopo ambayo inawanyima haki watoto wale kwa sababu wanaachwa wakiwa wadogo sana, wachanga, kiasi kwamba inaweza ikawasababishia vifo kwa kukosa uangalizi wa karibu wa mama?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili ni kwamba, Serikali sasa haini kwamba kwa kumnyima hizo haki mama yule ambaye amejifungua mtoto njiti wa siku zile za nyongeza kunaweza kukamsababishia matatizo ya afya ya akili ambayo itagharimu tena Serikali kumtibia matatizo ya afya ya akili ambayo yatamfanya asifanye kazi yake ipasavyo?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza yaliyoulizwa na Mheshimiwa Maimuna Mtanda, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na suala la kubadilsha sheria nataka nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge, sheria zipo, miongozo ipo na taratibu zipo. Changamoto inayotokea labda ni ile ambayo naweza kusema kwamba kuna baadhi ya Waajiri ambao kwa roho mbaya tu wanaamua kuwanyima hawa wazazi wanaopata watoto njiti. Lakini kwa upande wa sheria na zote zimeelezwa wazi, na mimi nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge pamoja na Bunge lako, lakini pia kutoa maelekezo kwa waajiri wote kwamba inapotokea mama amepata mtoto njiti na mazingira yanafahamika, watoto wanatakiwa kulelewa katika kangaroo basi ni wito wangu kwamba waongozwe pia na ubinadamu katika yale mamlaka ambayo wamepewa ili waweze kuwapa nafasi wazazi wakalee watoto wao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili katika maeneo ambayo kinamama may be labda wanakumbwa na hili tatizo ambalo Mheshimiwa Mbunge ameliita kwamba tatizo la afya ya akili; nataka nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge, sisi kama Serikali inayoongozwa na mwanamama Dkt. Samia Suluhu Hassan inawajali wakinamama Watanzania, inawajali watoto wa Tanzania lakini pia inatambua na kuheshimu na kulea afya za akili za Watanzania. Kwa hiyo nataka nikuhakikishie kwamba kama panapotokea matatizo hayo Mheshimiwa Rais ameishatoa maelekezo lakini pia na sisi tuwe chini yake tunamsadia, tumekwishapewa maelekezo na tunachotakiwa kufanya ni kuwaonea huruma wazazi hawa na kuwapa nafasi ili waende wakalee watoto wao ambao wamezaliwa katika mazinguru magumu kama hayo yaliyotajwa. (Makofi)

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENNEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri yanayotolewa na Naibu Waziri, Ridhiwani Kikwete nimesimama kwa sababu ya uzito la suala la watoto njiti. Wazazi wao wanapotakiwa wakimaliza siku 84 katika likizo ya uzazi, na bila shaka wote tunakubaliana kwamba siku 84 kwa mtoto aliyezaliwa njiti anakuwa bado hajaimarika sawa sawa; na unjiti unatofautiana, wengine wanazaliwa na miezi sita, wengine wanazaliwa miezi saba, wengine wanazaliwa miezi nane wanakuwa hawajakamilika uumbaji unakuwa bado unaendelea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kipo chama/NGO inayohusiana na masuala ya kusaidia watoto njiti, wamekwishaleta malalamiko mengi sana Serikali. Sasa leo nataka nionyeshe mahala ambapo Waheshimiwa Wabunge tusaidiane katika kuona kama tunahitaji kweli kubadilisha sheria au sheria iliyopo inajitosheleza kama ambavyo Mheshimiwa Naibu Waziri amejibu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisoma Kanuni za Utumishi wa Umma ya Mwaka 2009 Kanuni ya pili, H16 mnaweza mka-google hata nikimaliza kujibu swali mtapata maelezo yanayosema; “Except in cases of illness or other cases of emergence” yaani kwenye kesi hizi mtumishi ana haki ya kuomba extension of leave. Sasa tunajaribu kuona kama inatosha au haitoshi Waheshimiwa Wabunge, kwa sababu kundi hili ni kweli mtu akizaliwa anapofariki inaumiza sana na wengi humu tumezaliwa tukiwa njiti. Hatujisemi tu humu lakini tusingeangaliwa kwa zaidi ya siku 84 tungekuwa hatupo leo hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana tuipitie hiyo Kanuni halafu Waheshimiwa Wabunge wale wenye maoni, watatuletea maoni kama inatosha au haitoshi? (Makofi)

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA K.n.y. MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza siku za likizo kwa wazazi wanaojifungua watoto njiti?

Supplementary Question 2

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuweza kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa likizo ya uzazi ambapo wanaume wanapata siku tatu;

Je, Serikali haioni umefikia wakati kuongeza walau mwezi mmoja kwa wale wenza ambao watakuwa wamezaa watoto njiti? (Makofi)

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza lililoulizwa na Mheshimiwa Toufiq Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake linaweza kuwa limejibiwa vizuri sana na Mheshimiwa Waziri wakati anatoa maelezo ya ziada katika majibu yangu niliyompa Mheshimiwa Mtanda. Na mimi nadhani ili nalo tuliunganishe katika maombi aliyotoa Mheshimiwa Waziri la kutoa maoni ili kuona kama kuna sababu ya kurekebisha baadi ya vifungu vilivyomo katika sheria na kanuni inayoongozwa masuala yote ya likizo hasa pia kwa wanaume ambao Mheshimiwa Toufiq anawapigia debe waongezwe zifike siku 30. (Makofi)

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA K.n.y. MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza siku za likizo kwa wazazi wanaojifungua watoto njiti?

Supplementary Question 3

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Pamoja na watoto njiti lakini pia kuna wanawake ambao wanajifungua watoto zaidi ya mmoja;

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwaongezea siku akina mama hawa ili angalau waweze kuweza kuwalea vizuri hawa watoto mpaka wanapofikia umri?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, labda nikiri mbele yako kwa kuwa mimi siyo mtalamu sana katika eneo hili analozungumza Mheshimiwa Mwaifunga, hasa anapofikia mama amezaa watoto zaidi ya mmoja au wawili au watatu kwa maana kwamba anahitaji kipindi gani ili aweze kupumzika. Lakini nataka nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Bunge lako, maelezo aliyotoa Mheshimiwa Waziri yatioshe kufungua ili boksi la mjadala wa hii sheria na kanuni ili tuweze kuona jinsi gani tunaweza tukarekebisha hasa tukiweka into consideration mawazo mazuri ya Mheshimiwa Mbunge Hawa Mwaifunga. (Makofi)