Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 48 Public Service Management Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 625 2023-06-14

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA K.n.y. MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza siku za likizo kwa wazazi wanaojifungua watoto njiti?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Agnes Elias Hokororo, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatoa likizo ya uzazi kwa watumishi kwa mujibu wa Kanuni H12 ya Kanuni za Kudumu katika Utumishi wa Umma ya mwaka 2009 ambapo pamoja na Kanuni Pili ya Kanuni ya 12 inabainisha kuwa muda wa likizo ya uzazi kwa mtumishi mwanamke ni siku 84 ambazo hutolewa mara moja katika kipindi cha miaka mitatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la kuongeza siku za likizo pale mtumishi anapojifungua mtoto njiti, suala hili halijawekewa utaratibu wa kikanuni kutokana na taratibu wa uendeshaji wa shughuli za Serikali. Hivyo, Mtumishi (Mzazi) anaweza kuomba ruhusa ya kawaida kutoka kwa Mwajiri wake inapotokea changamoto kama hiyo.