Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:- Je, Serikali ipo tayari kuwapandisha vyeo kwa mserereko kufikia daraja wanalostahili watumishi waliosubiri zaidi ya miaka 8 Kyerwa?

Supplementary Question 1

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Nishukuru Serikali kwa majibu yake. Wilaya ya Kyerwa tunayo mapungufu ya watumishi kwenye sekta ya elimu pamoja na sekta ya afya.

Je, lini Serikali itaongeza watumishi kwenye sekta hizo ambazo nimezitaja?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kuna watumishi 18 ambao wamestaafu mwaka 2018 wakiwemo watendaji wa kata, watumishi hawa mpaka sasa hivi bado hawajalipwa mafao yao. Nini tamko la Serikali juu ya watumishi hawa kulipwa mafao yao ili na wao waweze kufurahia utumishi ambao wametumikia Taifa hili?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyoeleza katika jibu langu la msingi kwamba Serikali imeendelea kupandisha madaraja watumishi wake pia imeendelea kuajiri watumishi katika maeneo ambayo yanahitajika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mapungufu aliyoyaeleza Mheshimiwa Mbunge nataka nimwahidi kwamba Serikali imeendelea kuyashughulikia na kwa mfano katika bajeti iliyopita ya mwaka 2022/2023 vibali vya ajira 30,000 vilitolewa na watumishi wote hawa waliajiriwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka unaofuta wa fedha ambao Bunge lako limetupitishia bajeti yetu tunatarajia kuajiri wafanyakazi au watumishi 45,000. Nataka nimwakikishie Mheshimiwa Mbunge pamoja na Bunge lako kwamba Serikali itaendelea kukabiliana na upungufu wa watumishi katika sekta zote zilizomo nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili anataka kujua juu ya watumishi 18 ambao hawajalipwa mafao. Nataka nimwombe Mheshimiwa Mbunge kwamba watumishi hao kama hawajaleta barua katika Ofisi ya Katibu Mkuu Utumishi basi barua zao zifike haraka na kama wameshazileta baada ya hapa naomba nipate taarifa zaidi ili niweze kuyafatilia.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:- Je, Serikali ipo tayari kuwapandisha vyeo kwa mserereko kufikia daraja wanalostahili watumishi waliosubiri zaidi ya miaka 8 Kyerwa?

Supplementary Question 2

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipatia nafasi ya swali la nyongeza. Serikali mwaka jana ilipandisha vyeo au madaraja watumishi katika sekta ya umma baada ya kushindwa kupandishwa kwa takribani miaka mitano. Upandishwaji huu umesababisha changamoto ya walioajiriwa mwanzo na walioajiriwa baadaye wote kujikuta wapo katika kundi moja au daraja moja. Nini tamko la Serikali kutoa maelekezo kwa mamlaka za ajira nchini ikiwemo Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa ili ifanye uchambuzi na hatimaye walioajiriwa wakiwa daraja moja waweze kuwekwa katika madaraja stahiki?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ally Kassinge Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua kwamba kuwapandisha vyeo watumishi ni sehemu ya kuwapa motisha ili waendelee kufanya kazi vizuri pia ni eneo la kuendelea kusimamia usimamizi wa watumishi wa umma katika nchi yetu. Nataka nimwakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hapo mapungufu yaliyojitokeza katika utumishi ambayo yanahitaji watu wapandishwe vyeo yote tunayafanyia kazi na tutaendelea kutoa taarifa kadiri tunavyoendelea kupata nafasi ya kufanya hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hilo nataka nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba taarifa za watumishi wako zote ambao wana malalamiko kama hayo kupitia wewe tungependa tuzipate Serikali ili tuweze kuzifanyia kazi na kuweza kuwapatia haki yao wafanyakazi hao.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:- Je, Serikali ipo tayari kuwapandisha vyeo kwa mserereko kufikia daraja wanalostahili watumishi waliosubiri zaidi ya miaka 8 Kyerwa?

Supplementary Question 3

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kupata fursa hii kuuliza swali la nyongeza. Katika Halmashauri ya Mji wa Bunda kuna walimu takribani 28 wamekuwa wakikwama kupandishwa madaraja na ili hali kuna wenzao wamekuwa wakipandishwa madaraja kila mwaka walioajiriwa kwa mwaka mmoja. Tumelifuatilia suala hili wanasema tatizo ni mfumo na mimi nimechukua hatua ya kumpigia Katibu Mkuu Utumishi. Ningependa kujua ni lini sasa tatizo hili litaisha kwa hawa walimu 28 wa Halmashauri ya Mji wa Bunda ili waweze kupata haki yao kama wengine?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ester Bulaya, Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, maelekezo ya Serikali ni kwamba watumishi wote wanaostahili kupandishwa vyeo wapandishwe kwa mujibu wa taratibu kama nilivyoeleza kwenye swali la msingi. Na hapa nakusudia na nimaelekezo ya Serikali, kwamba kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Bunda Mji na viongozi wote katika Halmashauri nyingine zote Tanzania, maelekezo ya Serikali yako wazi na wayafate na kutotii maelekezo hayo ni kutotii uelekezo halali ya Mheshimiwa Rais, ambayo ameelekeza katika, alipokuwa anatoa maelekezo tarehe 19 Aprili, kwamba anataka wafanyakazi wote wanaostahili kupandishwa vyeo wapandishwe vyeo, wanatakiwa kufanyiwa recategorization wafanyiwe recategorization, lakini pia wale ambao kwa muda mrefu sana wamekuwa wanasubiri kuajiliwa nao pia wenye sifa za kuajiriwa, waajiriwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo maelekezo haya yote nataka nikuhakikishie Bunge sisi kama Wizara au Ofisi ya Rais, TAMISEMI tunayasimamia hayo na ni maelekezo yetu kwamba tunataka halmashauri zote nazo zisimamie na kama kuna sehemu yeyote pamekwama basi wawasiliane na Ofisi ya Katibu Mkuu Utumishi ili kuweza kushughulikia changamoto zitakazokuwa zimejitokeza. (Makofi)

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:- Je, Serikali ipo tayari kuwapandisha vyeo kwa mserereko kufikia daraja wanalostahili watumishi waliosubiri zaidi ya miaka 8 Kyerwa?

Supplementary Question 4

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi ya kuuliza swali la nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali itoe kauli ya changamoto kubwa iliyopo ya mfanyakazi anapandishiwa mshahara vizuri kabisa lakini harekebishiwi mpaka anastaafu, na inampa matatizo ya kupata haki zake. Mheshimiwa hii ni changamoto kubwa naomba Serikali itoe kauli yake. (Makofi)

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Margaret Sitta Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kwanza kulihakikishia Bunge lako lakini pia kumuhakikishia Mbunge ndani ya Ofisi ya Rais, TAMISEMI tunayo idara maalum inayohusika na masuala ya marupurupu, mishahara na nyongeza zote ambazo ni stahiki za mtumishi anatakiwa kupata. Sasa kama wapo watumishi ambao wanachangamoto katika hayo ofisi yetu iko wazi na ningeomba tupate taarifa hizo ili sasa tuweze kushughulikia na wafanyakazi wetu wote waweze kupata haki yao kama ambavyo imeelekezwa katika ratiba yetu. (Makofi)