Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 48 Public Service Management Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 624 2023-06-14

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:-

Je, Serikali ipo tayari kuwapandisha vyeo kwa mserereko kufikia daraja wanalostahili watumishi waliosubiri zaidi ya miaka 8 Kyerwa?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi na Utawala Bora, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Innocent Sebba Bilakwate, Mbunge wa Kyerwa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, upandishwaji vyeo kwa mserereko ni utaratibu unaotumika kuwapandisha vyeo watumishi ambao imethibitika kuwa walicheleweshwa kupandishwa vyeo kwa wakati kwa kuzingatia miongozo ya upandishaji vyeo iliyopo, uwepo wa nafasi iliyoidhinishwa katika Ikama na uwepo wa fedha za kugharamia upandishwaji vyeo kwenye bajeti, sifa za kielimu na kitaaluma na utendaji kazi mzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa msingi wa maelezo hayo, Serikali itakuwa tayari kuwapandisha vyeo kwa mserereko watumishi waliotajwa na Mheshimiwa Mbunge endapo itathibitika kuwa wana sifa zilizoainishwa.