Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza:- Je, nini hatma ya Barabara ya Zakhiem Mbagala Kuu inayoshindwa kujengwa kwa kuwa bomba la mafuta lipo chini ya barabara?

Supplementary Question 1

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na umuhimu wa barabara na kwa kuwa nyumba zilizo mbele ya Barabara hii, viwanja vyake vilipimwa na mamlaka ya upangaji.

Je, Serikali ina mpango gani wa kufidia walau mita sita ili wananchi wa eneo hili wapate Barabara ya uhakika?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili nini hatma ya barabara ya Mabwawa ya Samaki na Mlima habarizenu iliyopo katika Kata ya Mianzini?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Abdallah Chaurembo. La kwanza hili la kipande cha mita 400 kilichosalia katika barabara hii ya Zakhiem.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara hii kwa kumbukumbu zangu ni barabara ambayo inaunganika na maandazi road ambayo barabara hii ya Maandazi Road imewekwa katika mpango wa DMDP II. Sasa kwa sababu ni mita chache kutoka pale tutakaa na wenzetu wa Manispaa ya Temeke na vilevile tutakaa na wenzetu wa TARURA Mkoa wa Dar es Salaam kuona ni namna gani tunaweza tukachepusha barabara hizi mita 200 kwa kuona kama tunaweza kuingiza katika mpango wa kulipa fidia. Halmashauri wenyewe baada ya kufanya tathmini walipe fidia kwa ajili ya kuchepusha barabara hii ili iweze nayo kuingizwa katika mipango ya kuwekewa lami au zege ili wananchi hawa waweze kupata huduma sahihi wanayostahili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye swali lake la pili, barabara hii aliyoitaja ya Bwawa la Samaki hadi Kilima cha Habaribzenu. Naomba nitumie nafasi hii kumwelekeza Meneja wa TARURA wa Halmashauri ya Wilaya ya Temeke kufika katika barabara hii na kuweza kufanya tathmini na kuona ni namna gani inaweza ikatengewa fedha ya kuweza kutengeneza ili iweze kupitika wakati wote.

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza:- Je, nini hatma ya Barabara ya Zakhiem Mbagala Kuu inayoshindwa kujengwa kwa kuwa bomba la mafuta lipo chini ya barabara?

Supplementary Question 2

MHE. JERRY W. SILAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi kuuliza swali moja la nyongeza. Mvua za masika zimekuwa ni ndefu sana kwenye Mkoa wa Dar es Salaam na miundombinu mingi ya barabara imeharibika. Tarehe 30 Mei Mheshimiwa Naibu Waziri aliniahidi kwamba Barabara ya Banana-Kitunda-Kivule - Msongola itapitika na hali bado ni mbaya ikiwemo Barabara ya kwa Diwani – Bomba mbili. Nini kauli ya Serikali kuhusiana na miundombinu hii ya Jimbo la Ukonga ambayo ina hali mbaya kwa sasa?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jerry William Silaa naomba nitumie nafasi hii kumwelekeza Meneja wa TARURA Mkoa wa Dar es Salaam aweze kutembelea barabara hizi ambazo amezitaja Mheshimiwa Jerry William Silaa na kufanya tathmini ya haraka na pale tunapoanza utekelezaji wa bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024 kuzipa kipaumbele barabara hizi kwa ajili ya kuzitengeneza.

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza:- Je, nini hatma ya Barabara ya Zakhiem Mbagala Kuu inayoshindwa kujengwa kwa kuwa bomba la mafuta lipo chini ya barabara?

Supplementary Question 3

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana swali langu ni dogo tu kusiana kama lililokuwa Mbagala. Iko barabara inayopita ndani ya Jimbo la Temeke, sawa sawa na sambamba na Reli ya TAZARA ambayo nayo katika mvua hizi imeharibika sana.

Je, Serikali mtatusaidiaje changamoto ya TAZARA pamoja na Manispaa yetu ili waturuhusu hata kuitengeneza tu kwa changarawe au hata kuweka lami kidogo kwa sababu ni Barabara ambayo inatumika sana kwa wananchi wa Temeke.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii alimradi inapita kandokando mwa reli kuna sheria ambazo zinalinda ile mipaka ya reli inakopita. Hivyo tutakaa na wenzetu wa TAZARA kuona ni namna gani wataruhusu ipitike kwa muda kwa sababu haitoweza kutengenezewa miundombinu kama ya zege na lami kwa muda ili kuweza kutoa huduma kwa wananchi na TAZARA wakiridhia basi tutaona ni namna gani Meneja wa TARURA Mkoa wa Dar es Salaam anaweza akatengea fedha kwa ajili ya kuweza kuweka changarawe.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza:- Je, nini hatma ya Barabara ya Zakhiem Mbagala Kuu inayoshindwa kujengwa kwa kuwa bomba la mafuta lipo chini ya barabara?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafsi niulize swali la nyongeza. Je, lini Serikali italeta fedha kwa ajili ya ujenzi wa Barabara ya Ilula, Ibumu ili ijengwe japo kwa kiwango cha changarawe tu na madaraja manne ili wananchi waweze kupita, manake sasa hivi wanapata mateso makubwa sana.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, tutakaa na Mheshimiwa Kabati kuona kama barabara hii ya Ilula - Igumu imewekwa katika mradi wa Agri-connect ambao wao Iringa ni wanufaika wa mradi huu. Kama haijawekwa basi kuona ni namna gani bajeti ya TARURA ya Wilaya ya Kilolo inaweza ika-accommodate barabara hii katika mwaka wa fedha unaofuata na kama sio mwaka wa fedha unaofuata basi ule wa 2024/2025.

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza:- Je, nini hatma ya Barabara ya Zakhiem Mbagala Kuu inayoshindwa kujengwa kwa kuwa bomba la mafuta lipo chini ya barabara?

Supplementary Question 5

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana swali langu ni dogo tu kusiana kama lililokuwa Mbagala. Iko barabara inayopita ndani ya Jimbo la Temeke, sawa sawa na sambamba na Reli ya TAZARA ambayo nayo katika mvua hizi imeharibika sana.

Je, Serikali mtatusaidiaje changamoto ya TAZARA pamoja na Manispaa yetu ili waturuhusu hata kuitengeneza tu kwa changarawe au hata kuweka lami kidogo kwa sababu ni Barabara ambayo inatumika sana kwa wananchi wa Temeke.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii alimradi inapita kandokando mwa reli kuna sheria ambazo zinalinda ile mipaka ya reli inakopita. Hivyo tutakaa na wenzetu wa TAZARA kuona ni namna gani wataruhusu ipitike kwa muda kwa sababu haitoweza kutengenezewa miundombinu kama ya zege na lami kwa muda ili kuweza kutoa huduma kwa wananchi na TAZARA wakiridhia basi tutaona ni namna gani Meneja wa TARURA Mkoa wa Dar es Salaam anaweza akatengea fedha kwa ajili ya kuweza kuweka changarawe.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza:- Je, nini hatma ya Barabara ya Zakhiem Mbagala Kuu inayoshindwa kujengwa kwa kuwa bomba la mafuta lipo chini ya barabara?

Supplementary Question 6

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafsi niulize swali la nyongeza. Je, lini Serikali italeta fedha kwa ajili ya ujenzi wa Barabara ya Ilula, Ibumu ili ijengwe japo kwa kiwango cha changarawe tu na madaraja manne ili wananchi waweze kupita, manake sasa hivi wanapata mateso makubwa sana.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, tutakaa na Mheshimiwa Kabati kuona kama barabara hii ya Ilula - Igumu imewekwa katika mradi wa Agri-connect ambao wao Iringa ni wanufaika wa mradi huu. Kama haijawekwa basi kuona ni namna gani bajeti ya TARURA ya Wilaya ya Kilolo inaweza ika-accommodate barabara hii katika mwaka wa fedha unaofuata na kama sio mwaka wa fedha unaofuata basi ule wa 2024/2025.