Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 48 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 623 2023-06-14

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza:-

Je, nini hatma ya Barabara ya Zakhiem Mbagala Kuu inayoshindwa kujengwa kwa kuwa bomba la mafuta lipo chini ya barabara?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu Swali la Mheshimiwa Abdallah Jafari Chaurembo, Mbunge wa Jimbo la Mbagala kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara ya Kijichi - Mbagala Kuu - Zakhiem ina urefu wa kilometa 5.1. Kati ya kilometa hizo kipande cha mita 600 ni sehemu ya bomba la mafuta la TAZAMA. Baada ya majadiliano ya mara kwa mara kati ya TARURA, TAZAMA na Halmashauri ya Manispaa ya Temeke, TAZAMA waliruhusu mita 200 kuwekewa tabaka la zege na tayari tabaka la zege limewekwa kwa gharama ya shilingi milioni 155.79 kupitia mradi wa DMDP.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kipande cha mita 400 kilichobaki, TAZAMA wameruhusu kiwekewe tabaka la changarawe pekee na sio kujenga barabara kwa kiwango cha lami au zege.