Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE K.n.y. MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza:- Je, lini Serikali itatoa fedha kumalizia ujenzi wa Vituo vya Afya Matwiga na Mafyeko Jimboni Lupa?

Supplementary Question 1

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa niaba ya Mheshimiwa Masache nashukuru sana Serikali kwa majibu mazuri na tunaamini wananchi wa Lupa kwenye mgawanyo wa magari watapata. Naomba sasa niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza lini Serikali itapeleka fedha za kumalizia ujenzi wa kituo cha afya Masamakati na Mkwansira?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili wananchi wa Kata ya Rom pamoja na ufinyu wa maeneo wamehangaika sana wamepata eneo la kujenga kituo cha afya pale Rowsinde. Je, lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya kujenga kituo cha afya?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kasaka yaliyoulizwa kwa niaba yake na Mheshimiwa Mbunge wa Hai rafiki yangu Saashisha Elinikyo Mafuwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza la lini Masamakati itapelekewa fedha? Naomba nijibu haya maswali mawili kwa pamoja hili la kwanza na la pili. La kwanza ni kuwataka wao Halmashauri ya Wilaya ya Hai kuanza kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa vituo hivi vya afya vya Rowsinde na hichi ambacho cha Masamakati. Pale watakapokuwa wanakwenda na kukitengea fedha katika bajeti zao ndipo napo Serikali wakati tunatafuta fedha ya kuendelea kujenga vituo vya afya, tunaona ni namna gani tutakuja kuongeza nguvu za halmashauri walikofikia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali hii ya awamu ya sita ya mama Samia Suluhu Hassan imejenga vituo vya afya 234 kote nchini kwa kutenga bilioni 116 na tayari vituo hivyo vingi vimeshakamilika na kuanza kazi. Sasa ni wajibu wa halmashauri hizi nazo ku-support jitihada hizi za Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuweka fedha kwa ajili ya ujenzi huu kwa wao kuanza ujenzi wa vituo hivi vya afya. Naamini kule wenzetu wa Hai nao watakaa halmashauri na kuweka fedha kwa ajili ya kuanza kupeleka huduma ya wananchi huku.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitumie nafasi hii vilevile kumwelekeza Mganda Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro kwenda kufanya tathmini katika maeneo haya aliyoyataja Mheshimiwa Saashisha na kuona idadi ya wananchi waliokuwepo pale, uhitaji uliopo kwa ajili ya kupata vituo hivi vya afya na kuwasilisha taarifa ile Ofisi ya Rais TAMISEMI.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE K.n.y. MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza:- Je, lini Serikali itatoa fedha kumalizia ujenzi wa Vituo vya Afya Matwiga na Mafyeko Jimboni Lupa?

Supplementary Question 2

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante Tarafa ya Mlalo yenye kata nne inahitaji kituo kimoja cha kimkakati ambacho kitahudumia Kata ya Lukozi, Malindi, Manolo na Shume.

Je, Serikali ina mpango gani kujenga kituo hiki kwa haraka kwa sababu pia ni ahadi ya Mheshimiwa Waziri Mkuu alipofanya ziara katika Kata ya Lukozi?

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru nipende kujibu swali la Mheshimiwa Shangazi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nimshukuru kwa namna ambavyo ameendelea kufuatilia maendeleo ya jimbo lake lakini kwa namna ambavyo ameendelea kufatilia utekelezaji wa ahadi za viongozi wetu. Nipende tu kumwakikishia kwamba tunatambua umuhimu na namna ambavyo Kata hii ya Lukozi iko kimkakati. Tunajua kituo hichi endapo kitajengwa kitaweza kuhudumia zaidi ya kata nne ikiwemo Manolo, Malindi, Lukozi yenyewe na nimpe tu uhakika. Kwamba tutakijenga katika mwaka ujao wa fedha 2023/2024 kama ambavyo tutaweza kupanua Kituo cha Afya cha Mlalo vilevile katika Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto kwa Mheshimiwa Shekilindi tutaweza pia nako kujenga kituo cha afya kwa upande Gare, nikushukuru.

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE K.n.y. MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza:- Je, lini Serikali itatoa fedha kumalizia ujenzi wa Vituo vya Afya Matwiga na Mafyeko Jimboni Lupa?

Supplementary Question 3

MHE. ATHUMAN A. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kunipa mimi ruhusa ya kuuliza swali la mwisho la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Kata ya Chitage na Kata ya Usagari Mbunge kwa kushirikiana na wananchi tunajenga vituo vya afya.

Je, Serikali ina mpango gani wa kutusaidia kumalizia vituo hivyo vya Chitage na Usagari Mikungumalo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nitumie nafasi hii kwanza kumpongeza Mheshimiwa Almas Maige yeye pamoja na wananchi wake kuweza kujitoa kuanza ujenzi wa vituo hivi vya afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba vilevile nimtake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tabora kufika katika vituo hivi vya afya ambavyo vimeanza kujengwa kwa nguvu ya wananchi na kufanya tathmini na kuona vile vigezo ambavyo vinahitajika kwa ajili ya kusajili kituo cha afya kama wanakidhi hawa wananchi wa Mheshimiwa Maige na wawasilishe taarifa hiyo Ofisi ya Rais TAMISEMI ili tuviweke katika mipango yetu ya utafutaji wa fedha katika Ofisi ya Rais-TAMISEMI.

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE K.n.y. MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza:- Je, lini Serikali itatoa fedha kumalizia ujenzi wa Vituo vya Afya Matwiga na Mafyeko Jimboni Lupa?

Supplementary Question 4

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona, wananchi wa Mji wa Mafinga walishaanza kujenga Kituo cha Afya cha Upendo na kwa nguvu zao wenyewe.

Ni lini Serikali itapeleka nguvu za ujenzi katika kituo hicho?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itapeleka fedha katika Kituo hicho cha Afya Upendo ku-support nguvu za wananchi kadiri ya upatikanaji wa fedha. Vilevile nao wana uwezo wa kuanza kutenga bajeti kwa ajili ya ku-support jitihada hizi za wananchi hawa.

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE K.n.y. MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza:- Je, lini Serikali itatoa fedha kumalizia ujenzi wa Vituo vya Afya Matwiga na Mafyeko Jimboni Lupa?

Supplementary Question 5

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi. Je, lini Serikali itapeleka fedha za kutosha kumalizia Kituo cha Afya cha Makuro Jimbo la Singida Kaskazini?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itapeleka fedha za kumalizia Kituo cha Afya Makuro kadiri ya upatikanaji wa fedha na tutakaa na Mheshimiwa Mbunge kuona kama kimetengewa fedha katika mwaka wa fedha ujao.

Name

Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE K.n.y. MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza:- Je, lini Serikali itatoa fedha kumalizia ujenzi wa Vituo vya Afya Matwiga na Mafyeko Jimboni Lupa?

Supplementary Question 6

MHE. TUMAINI B. MAGESSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Je, lini Serikali itajenga vituo vya afya kwenye Kata za Rwamgasa, Nyakagomba na Magenge tulizoziomba mwaka 2021?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itajenga vituo vya afya hivi alivyovitaja Mheshimiwa Magessa kadiri ya upatikanaji wa fedha.