Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza:- Je, lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga barabara za lami katika Mji wa Mombo?

Supplementary Question 1

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, ujenzi wa barabara za lami kilometa tatu kwenye Mji wa Mombo ni ahadi ya Serikali iliyotolewa na Mgombea wa Urais wa Chama cha Mapinduzi mwaka 2015 na ikarejewa mwaka 2022. Kazi inayoendelea haiathiri ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami, nataka kujua, ni lini ahadi hii ya Serikali kwenye Mji wa Mombo itatekelezwa? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Wilaya ya Korogwe ni eneo muhimu sana kwenye uzalishaji wa mazao ya kilimo, kilimo cha mkonge lakini Tarafa ya Bundi kilimo cha chai: Ni lini Serikali itaiingiza Wilaya ya Korogwe kwenye mradi ule mahususi wa miundombinu kwenye maeneo ya uzalishaji na maeneo ya kilimo? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Timotheo Mnzava, Mbunge wa Korogwe Vijijini, la kwanza hili kwamba barabara hii ya lami ni ahadi ya Serikali, nikiri kwamba ni ahadi ya Serikali na kwamba tutaendelea kuipa kipaumbele kwa sababu iliahidiwa na Kiongozi Mkuu wa Nchi alipopita katika eneo la Mombo. Tutaendelea kutafuta fedha na tutaona ni namna gani katika mwaka wa fedha huu tunaoenda kuuanza ni nini kinaweza kikafanyika na Serikali kuweza kuendelea kutekeleza ahadi hii ya viongozi wakuu wa Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye swali lake la pili kwamba kule kuna uzalishaji mkubwa kuingiza katika miradi mbalimbali mingine, nimtoe mashaka, Korogwe vijijini ipo katika mradi ule wa bottleneck removal ambao unakwenda kujenga madaraja na vivuko mbalimbali katika maeneo tofauti hapa nchini, ikiwemo kule kwake Mheshimiwa Mnzava, Korogwe Vijijini. Najua alichokuwa anataka ni kwamba Mkoa wa Tanga wawekwe katika Mradi wa Agri-connect, lakini mradi huu wa Agri-connect upo katika Southern Highlands, mikoa yetu ya nyanda za juu kusini tu, na wao Korogwe wapo katika hii bottleneck removal kwa vijijini; kwa Korogwe Mjini, kwa Dkt. Kimea kule, wamo katika TACTIC na Tanga Mjini vile vile wapo katika TACTIC.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tutaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kufanya ukarabati na matengenezo ya barabara mbalimbali kule Korogwe Vijijini.

Name

Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza:- Je, lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga barabara za lami katika Mji wa Mombo?

Supplementary Question 2

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nami ninalo swali linalofanana na Korogwe. Pale Mji wa Nguruka Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano aliwaahidi kilometa tano za lami, lakini mpaka sasa zimejengwa mita 250 tu. Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya kujenga barabara za lami pale Nguruka? Ahsante. (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Nashon kwenye hii barabara ya Nguruka ambayo ni ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tutakaa kupitia ahadi zote za Viongozi Wakuu, kupitia wakala wetu wa TARURA na kuona ni namna gani tunaweza tukakaa na wenzetu wa Wizara ya Fedha kwa ajili ya kuona tunapataje fedha ya kuanza kutengeneza taratibu kutenga ili kila mwaka angalau kwenye ahadi hizi tuweze kuwa tunapunguza kilometa hizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimtoe mashaka Mheshimiwa Mbunge, kwamba tunalifanyia kazi chini ya Waziri wetu Mheshimiwa Angellah Kairuki, kuhakikisha kwamba tunajua ahadi zote na kuziratibu na kuhakikisha barabara hizi zinajengwa kwa wakati.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza:- Je, lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga barabara za lami katika Mji wa Mombo?

Supplementary Question 3

MHE. JAPEHT N. HASUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Barabara ya Vwawa – London – Iganduka hadi Msiya hivi sasa haipitiki kabisa; Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba barabara hiyo inawekwa lami ili iweze kupitika wakati wote?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali la Mheshimiwa Hasunga la Barabara zake hizi za Vwawa kuwekewa lami. Nitakaa naye Mheshimiwa Hasunga kuona ni kiasi gani kimetengwa katika mwaka wa fedha 2023/2024 katika jimbo lake kule ili tuweze kuhakikisha kwamba upatikanaji wa fedha huu unakuwa wa haraka na hizi ziweze kuanza kujengwa mara moja na kama hazijatengewa fedha basi tutahakikisha na Mheshimiwa Hasunga tutakaa naye kuona zinatengewa fedha katika mwaka wa fedha wa 2024/2025.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza:- Je, lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga barabara za lami katika Mji wa Mombo?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana, je lini Serikali itajenga Barabara ya Mikumi, Kisanga, Maroro kwa kiwango wa changarawe? Ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itajenga Barabara hii ya Mikumi, Kisanga kama ambavyo ameuliza Dkt. Ishengoma kadiri ya upatikanaji wa fedha na tutaangalia katika mwaka wa fedha huu unaoanza, ambapo TARURA vile Bunge hili lilipitishia bajeti kubwa ya kuweza kutekeleza barabara hizi kuona kama imetengewa fedha na kama haijatengewa fedha tutaangalia katika mwaka wa fedha unaofuata ili barabara hii iweze kutengewa fedha.

Name

Daniel Awack Tlemai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza:- Je, lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga barabara za lami katika Mji wa Mombo?

Supplementary Question 5

MHE. DANIEL A. TLEMAI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante je, lini Serikali itatekeleza ahadi ya kilometa 10 katika Mji wa Karatu?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nitakaa naye Mheshimiwa Mbunge kwa sababu bado sijaelewa ahadi hii ilikuwa iko vipi. Nitakaa naye Mheshimiwa Mbunge ili aweze kunielewesha vizuri ahadi hii ya kilometa 10 ilikuwa ni ahadi ipi na tuweze kujua kama ni ya TANROADS au ni ya kwetu halafu tuone ni namna gani tunaweza tukapata fedha ya kuanza kutekeleza walau kwa kilometa moja moja ili iweze kukamilika kule Karatu.