Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 48 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 621 2023-06-14

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza:-

Je, lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kujenga barabara za lami katika Mji wa Mombo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Timotheo Paul Mnzava, Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2021/2022, TARURA ilitenga jumla ya kiasi cha shilingi milioni 200 kwa ajili ya kuchonga na kuweka changarawe urefu wa kilometa 2.7, kujenga makalavati tisa, kujenga mifereji yenye urefu wa kilometa 1.9. Aidha, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imetenga jumla ya Shilingi milioni 400 kwa ajili ya kuchonga kilometa 2.84 kwa kuweka changarawe, ujenzi wa makalavati 23 na ujenzi wa mifereji urefu wa kilometa 2.46. Utekelezaji wa kazi hizi unaendelea na umefikia asilimia 56. Kwa mwaka wa fedha 2023/2024 jumla ya shilingi milioni 200 zimetengwa kwa ajili ya barabara hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara za Mombo Mjini zitaanza kujengwa kwa kiwango cha lami mara baada ya kuziimarisha kwa kiwango cha changarawe na ujenzi wa mifereji kulingana na upatikanaji wa fedha.