Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga Barabara ya Mogitu – Dawar hadi Ziwa Chumvi ili kusafirisha chumvi ghafi kwenda kiwandani?

Supplementary Question 1

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza naishukuru sana Serikali kwa fedha ambazo zimewekwa kwa ajili ya barabara ya Mogitu – Dawar – Ziwa Chumvi, lakini pia kwa shilingi milioni 53 ambayo imetengwa kwa ajili ya Dawar – Endasak. Pamoja na pongezi hizo, nina maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza maeneo ya Mara – Getaqul ambayo iko Kata ya Measkron, na Merekwa – Gauror ambayo iko Kata ya Dirima na Sosomega ambayo iko Kata ya Hirbadaw kipindi cha mvua huwa yanakuwa kama yako kisiwani.

Je, Serikali ina mkakati gani wa haraka kufikisha mkono wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan maeneo hayo ili nao waweze kufurahia maisha kwenye eneo hilo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; tuna changamoto kubwa ya daraja kule Sirop. Serikali imeshatenga fedha shilingi milioni 568; je, ni lini ujenzi wa daraja hilo utaanza ili wananchi waachane na adha ya daraja hilo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Hhayuma. Swali lake la kwanza hili la Kata ya Dirima aliyotaja na vijiji ambapo barabara hizi zipo katika kata ambayo mvua ikinyesha wanakuwa wako kisiwani, naomba nichukue nafasi hii mbele ya Bunge lako Tukufu kumwelekeza Meneja wa TARURA wa Wilaya ya Hanang’ kwenda kufanya tathmini ya barabara hii na kisha kuiwasilisha Makao Makuu ya TARURA ili kuona ni namna gani tunaweza tukai-accommodate katika bajeti zifuatazo kuitengeneza barabara hii ili wananchi hawa wasiwe kisiwani kipindi cha mvua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye swali lake la pili. Kwanza nimpongeze Mheshimiwa Hhayuma kwa sababu amekuwa akifuatilia sana upatikanaji wa fedha wa daraja hili ambalo linaenda kujengwa kwa Shilingi milioni 568 ambalo amelitaja yeye mwenyewe, nimhakikishie kwamba mara tu tutapoanza mwaka wa fedha wa 2023/2024 ujenzi huu utaanza kwa kutangaza kazi hii ili apatikane kandarasi kwa ajili ya kujenga daraja hili.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga Barabara ya Mogitu – Dawar hadi Ziwa Chumvi ili kusafirisha chumvi ghafi kwenda kiwandani?

Supplementary Question 2

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi. Mheshimiwa Naibu Waziri, barabara ya kutoka Korongo kwenda Utinta imekuwa na changamoto kubwa sana na kuleta hatari kwa wanafunzi: Ni lini mtawaongezea fedha TARURA ili waweze kujenga kipande hicho?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Aida Khenani, Serikali imeongezea fedha TARURA ukilinganisha mwaka wa fedha 2020/2021 na 2021/2022, 2022/2023 na hata 2023/2024 tunayoenda kutekeleza, TARURA wameongezewa zaidi ya mara tatu ya bajeti ambayo ilikuwepo hapo awali. Kwa hiyo, ni kukaa na Meneja wa TARURA wa Mkoa kuangalia ni kiasi gani kimetengwa kwa ajili ya kukarabati vile vile eneo la Wilaya ya Nkasi anakotoka Mheshimiwa Khenani ambapo wanafunzi wanavuka kama ambavyo amesema Mheshimiwa Mbunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba vile vile Meneja wa Wilaya ya Nkasi awasilane na Mheshimiwa Khenani ili kuona ni namna gani wanaweza wakaanza ukarabati wa barabara hii.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga Barabara ya Mogitu – Dawar hadi Ziwa Chumvi ili kusafirisha chumvi ghafi kwenda kiwandani?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Katika Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu DC Barabara ya Mgombe – Kagerankanda mpaka Mvinza ni barabara ya kiuchumi na hupitisha malori makubwa kwenda kuchukua chokaa kupeleka nchi jirani ya Burundi; je, ni lini Serikali itajenga barabara hiyo? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii ambayo ameiulizia Mheshimiwa Genzabuke kwenye swali lake la nyongeza, ni barabara ambayo inaambaa ambaa pembezoni mwa Mto Malagarasi. Kule wanaenda kufuata clinker ambayo inatengenezea madini ya ujenzi (cement). Kwa hiyo, tunaiona changamoto hii iliyopo kwa sababu mwanzo wakati barabara hii inahudumiwa na TARURA kulikuwa bado hakuna malori mengi yanayopita yenye uzito mkubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa kwa sababu malori tayari ni mengi sana, tutakaa na wenzetu wa TANROADS kuona ni namna gani ambapo wao wenyewe wataanza kwanza kule Kasulu kuona ni namna gani wanapandisha hadhi barabara hii kuwa barabara ya TANROADS ili iweze kuhudumiwa kwa ubora zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwongezee tu Mheshimiwa Mbunge kwamba hata Mamlaka ya Bandari Tanzania nayo ilikuwa inaangalia uwezekano wa kupanua mto ule ili zile barge kubwa ziweze kuwa zinapita kuchukua ile clinker badala ya kupitisha kwenye barabara zile.

Name

Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga Barabara ya Mogitu – Dawar hadi Ziwa Chumvi ili kusafirisha chumvi ghafi kwenda kiwandani?

Supplementary Question 4

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniruhusu niulize swali la nyongeza. Kwa sababu ya wingi wa mvua zinazonyesha katika Jiji la Dar es Salaam, barabara nyingi zilizo chini ya TARURA katika Jimbo la Kawe zimekatika vipande vipande.

Ni nini mpango wa Serikali ku-repair barabara hizi ili wananchi waweze kupita na kuondoa usumbufu? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Gwajima la barabara za Dar es Salaam kukatikakatika kwa sababu ya mvua, tunaenda kuanza kutekeleza Bajeti ya mwaka 2023/2024 kwa Wakala wa barabara ikiwemo Dar es Salaam. Mheshimiwa Mbunge naye ni shahidi kwamba hivi karibuni wamesaini mkataba kwa ajili ya uanzishwaji wa mradi wa DMDP II ambao utakwenda kuwa mwarobaini wa barabara hizi mbovu za Jiji la Dar es Salaam kwa kujenga mifereji na kuhakikisha barabara pia zinapitika wakati wote.