Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 48 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 619 2023-06-14

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza:-

Je, lini Serikali itajenga Barabara ya Mogitu – Dawar hadi Ziwa Chumvi ili kusafirisha chumvi ghafi kwenda kiwandani?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Samweli Hhayuma, Mbunge wa Jimbo la Hanang’ kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha wa 2022/2023, shilingi milioni 188.73 zimetumika kwa ajili ya kufungua na kujenga makalavati manne katika barabara ya Dawar – Ziwa Chumvi ambapo awali ilitumika kama njia ya ng’ombe (Pario). Ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha changarawe kwenye eneo la kilometa 6.3 umekamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha wa 2023/2024, Serikali imetenga shilingi milioni 53.34 kwa ajili ya kujenga kipande cha Barabara ya Endasak - Dawar inayoelekea Ziwa Chumvi chenye urefu wa kilometa nane.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kuihudumia Barabara ya Mogitu – Dawar mpaka Ziwa Chumvi kulingana na upatikanaji wa fedha.