Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza:- Je, ni faida gani ambayo Wafanyakazi wanapata kupitia uwekezaji wa fedha wanazokatwa na Vyama vya Wafanyakazi?

Supplementary Question 1

MHE. NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Mheshimiwa Naibu Waziri amekiri kwamba fedha za wafanyakazi zinaweka uwekezaji ambao unaendelea, yaani unafanyika uwekezaji mfano kujenga majengo ambayo yanaongeza kipato kwenye Vyama vya Wafanyakazi. Ninatamani kufahamu.

Ni lini Serikali itakuja na sheria ambayo inampa haki mwanachama yule kuweza kupata gawio kwa fedha zinazopatikanika kwa uwekezaji huo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili. Nataka kufahamu, kumekuwa na malalamiko mengi ya walimu kuhusiana na kulazimishwa kuingia kwenye vyama viwili viwili vya wafanyakazi: Ni nini kauli ya Serikali kuhakikisha kwamba kujiunga na uanachama wa Vyama vya Wafanyakazi ni hiari ili kusikuwepo na huko kulazimishana kuingia kwenye vyama viwili viwili hususan kwa walimu? Ahsante. (Makofi)

Name

Ummy Hamisi Nderiananga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE NA URATIBU (MHE. UMMY H. NDERIANANGA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, napenda nimjibu Mheshimiwa Neema Gelard Mwandabila na nimpongeze kwa kazi nzuri anayoifanya, lakini kwenye eneo hili la uwekezaji nimefafanua vizuri na sheria ipo ambayo inaviruhusu vyama hivi vya wafanyakazi, pia zipo kanuni ambazo zinawaongoza katika vyama vya kwa misingi ya katiba walizojiwekea. Kwa hiyo, nichukue tu kama maoni katika eneo hili, nitaonana naye baada ya hapa ili tuweze kuzungumza zaidi kuona nini hasa alimaanisha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile amesema kwamba wanachama wanalazimishwa kujiunga. Niseme kwamba vyama hivi ni vya hiari, lakini Katiba zao ndiyo ambazo zinawabana kwamba pengine ujiunge au ukijiunga atanufaika na nini na kipi? Kwa hiyo, siyo kwamba ni lazima kwamba lazima sasa ujiunge kwenye chama hiki. Hapana, lakini pia nitakutana naye tufahamiane zaidi ili tuone namna ya kuliweka vizuri, ahsante. (Makofi)

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza:- Je, ni faida gani ambayo Wafanyakazi wanapata kupitia uwekezaji wa fedha wanazokatwa na Vyama vya Wafanyakazi?

Supplementary Question 2

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Mheshimiwa Waziri katika vyama hivi ulazima upo, maana mfanyakazi hasa mwalimu anapoingia tu kwenye ajira anakatwa pesa bila yeye kuwa na ridhaa yake: Je, kama unasema siyo lazima, unaweza ukatoa tamko leo ili mwalimu yeyote aingie chama chochote anachokitaka yeye? (Makofi)

Name

Ummy Hamisi Nderiananga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE NA URATIBU (MHE. UMMY H. NDERIANANGA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kama nilivyojibu kwenye majibu yangu ya awali, nimesema zipo katiba ambazo zinavi-guide hivi vyama, kama pengine ni cha walimu au ni chama cha kada nyingine tofauti, wapo pale kwa mujibu wa katiba zao na makubaliano ambayo wanakubaliana wao kwa wao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunafahamu zipo baadhi ya changamoto pengine na migogoro katika vyama hivi. Serikali ya Awamu ya Sita chini Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan tutaendelea kufanya kazi kwa ukaribu na vyama hivi kuboresha upungufu ambao upo au kusuluhisha migogoro ambayo inaendelea katika vyama hivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niwatoe wasiwasi walimu, waendelee kukiamini Chama chao cha Walimu na sisi Serikali tuko pamoja nao. (Makofi)

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza:- Je, ni faida gani ambayo Wafanyakazi wanapata kupitia uwekezaji wa fedha wanazokatwa na Vyama vya Wafanyakazi?

Supplementary Question 3

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa kuwa wafanyakazi ni mali ya Serikali na Serikali ina wajibu kwa wafanyakazi hawa.

Je, haioni sasa umefika wakati mfanyakazi halazimishwi kujiunga kwenye chama bila hiari yake? Nadhani ni muhimu sana kutoa tamko hili Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)

Name

Ummy Hamisi Nderiananga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE NA URATIBU (MHE. UMMY H. NDERIANANGA): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumjibu Mheshimiwa Sima. Kama ambavyo nimejibu, amesema wafanyakazi ni mali ya Serikali. Nami niseme, tunawapongeza sana wafanyakazi wa Tanzania kwa kuendelea kufanya kazi kwa bidii kuliletea maendeleo Taifa letu, lakini tutaendelea kufanya mashauriano na kutoa ushirikiano na vyama hivi vya wafanyakazi ili waendelee kuwa na imani na vyama vyao na kuendelea kuliletea maendeleo. Ni mafanikio makubwa yamepatikana kupitia vyama hivi vya wafanyakazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mtaona hata Mheshimiwa Rais Dkt. Samia amepandisha madaraja, ameongeza fedha, anaendelea kupigania maslahi ya wafanyakazi. Kwa hiyo, niwatoe shaka wafanyakazi, tuko pamoja na tutaendelea kuwaratibu vizuri kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, ahsante. (Makofi)