Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 48 Policy, Coordination and Parliamentary Affairs Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge 618 2023-06-14

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza:-

Je, ni faida gani ambayo Wafanyakazi wanapata kupitia uwekezaji wa fedha wanazokatwa na Vyama vya Wafanyakazi?

Name

Ummy Hamisi Nderiananga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE NA URATIBU (MHE. UMMY H. NDERIANANGA) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Neema Gelard Mwandabila, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, faida ambayo wafanyakazi wanapata kupitia uwekezaji wa fedha wanazokatwa na Vyama vya Wafanyakazi ni pamoja na; Vyama vya Wafanyakazi kusuluhisha migogoro ya kikazi kwa niaba ya wanachama wake, kutoa huduma kwa wanachama kama vile ya utetezi katika Mahakama ya Kazi, na kutoa elimu kuhusu Sera na Sheria za kazi kwa ajili ya maslahi mapana ya wafanyakazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Vyama vya Wafanyakazi kupitia fedha wanazokusanya kutokana na ada za wanachama wao huzitumia kutekeleza majukumu ya vyama yaliyowekwa kikatiba na kisheria yanayotokana na uwepo wa vyama mahali pa kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vipo baadhi ya Vyama vya Wafanyakazi ambavyo hutumia ada za uanachama kujenga majengo kwa ajili ya matumizi ya ofisi za vyama, kuwapangisha watu mbalimbali na kutoa huduma kwa wanachama wao. Fedha inayopatikana kutokana na uwekezaji hutumika kuongeza bajeti za Vyama vya Wafanyakazi ili waweze kutekeleza majukumu yao ya kikatiba na kisheria kikamilifu, ahsante.