Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Munde Abdallah Tambwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUNDE T. ABDALLAH aliuliza:- Je, Serikali ina mpango mkakati gani kupitia diplomasia ya uchumi na nchi ya China kuunganisha wajasiriamali wadogo, wa kati na wakubwa ili kuingia ubia wa kuimarisha viwanda vidogo na vya kati?

Supplementary Question 1

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa fursa ya kuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.
Kwanza kabisa nianze kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri, lakini pia, niipongeze Serikali kwa kuonesha baadhi ya mikakati yao inayoendelea nayo na ninayo maswali mawili ya nyongeza. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, je, Serikali kupitia diplomasia yake ya kiuchumi nchini ina mkakati gani wa kuwashawishi wakulima wakubwa wa tumbaku nchini China waje kuingia ubia na wakulima wadogo wa tumbaku Mkoani Tabora, ili wakulima wa tumbaku Mkoani Tabora waweze kupata faida kubwa na yenye tija na kuona kilimo cha tumbaku sasa kinawasaidia, tofauti na hali ilivyo sasa? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa vijana wengi nchini wamejiajiri kwenye biashara ya bodaboda, hususan Mkoa wangu wa Tabora ambao vijana wengi wanaoendesha bodaboda hizo zisizo zao, je, Serikali kupitia diplomasia yake ya uchumi nchini inaweza leo kunihakikishia hapa kwamba, itafanya kila liwezekanalo kuhakikisha Mkoa wa Tabora unapata kiwanda cha pikipiki kutoka kwenye viwanda vikubwa kama SanLG, labda Boxer na viwanda vingine vyovyote vilivyopo China, ili kuweza kuwapatia vijana hawa pikipiki kwa bei nzuri, ili na sisi watu wa Mikoa ya Tabora, Katavi, Sumbawanga, Kanda ya Ziwa, tuweze kujikomboa kiuchumi kwa kupitia diplomasia hii? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Susan Alphonce Kolimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Spika, naomba nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Munde kwa kufanya kazi kubwa ya kuwatetea wananchi wa Tabora. Naomba niende kujibu maswali yake mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza ambalo linahusu jinsi Wizara yangu inaweza kufanya mkakati gani wa kuweza kuwezesha wakulima wakubwa wa China kujakuwekeza na kufanya kazi pamoja na wakulima wadogo wa Tabora.
Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Munde kwamba Wizara yangu ilifanya mkakati huo, sisi kama Wizara ni Wizara kiunganishi, tumefanya mkakati na mkakati huo ni kuwahakikishia kwamba watu wa China wanaweza wakawekeza katika zao la tumbaku na nimwambie tu kwa hali sasahivi ilivyo ni kwamba Balozi wa China nchini Tanzania pamoja na Wizara ya Kilimo wako katika mkakati wa majadiliano wa kuweza kufikia makubaliano ya kujua zao la tumbaku na bei ya tumbaku itakuwaje na sisi tumeaachia wao kama Wizara kwasababu sisi kazi yetu ni kuhakikisha kujenga mahusiano mazuri. Tukishawaleta, wakifika nchini tunawapeleka katika Wizara husika. Mheshimiwa Spika, kwahiyo, nikuhakikishie kwamba wakulima wa Tabora pamoja na wale wakulima wa China watafanya biashara hiyo ya tumbaku lakini baada ya mazungumzo na majadiliano yatakapokwisha kati ya Wizara ya Kilimo na Balozi wa China nchini Tanzania.
Mheshimiwa Spika, lakini la pili la kuhusu bodaboda na kuhusu vijana wa bodaboda waliopo Tabora na Kanda ya Ziwa, nikuhakikishie si tu Tabora na Kanda ya Ziwa lakini kwa Tanzania. Nafikiri umeshawahi kusikia ndani ya Bunge hili Waziri wa Viwanda na Biashara amezungumzia kuhusu suala la watu wa china kuwekeza katika viwanda vya kutengeneza bodaboda hapa Tanzania.
Kwa hiyo, biashara hiyo itakuwepo na watawezeshwa katika namna hiyo na kufundishwa pia jinsi ya kuendesha biashara ndogo ndogo kama ujasiriamali ili kusudi wasiwe tegemezi na waweze kutoka katika utegemezi na kufanya kazi yao vizuri.
Mheshimiwa Spika, niendelee kumhakikishia Mheshimiwa Munde kwamba sisi kama Wizara kwa kutumia diplomasia ya kiuchumi tutaendelea kupambania Tanzania iende katika kuhakikisha kwamba inatimiza ahadi yake ya kuhakikisha kwamba Tanzania inatoka katika hali ya kawaida na inakwenda katika uchumi wa viwanda.
Mheshimiwa Spika, tutatumia diplomasia hiyo kwa kutumia Mabalozi wetu wote waliopo nje na wale waliopo Tanzania na kutumia vijana wetu na watumishi wetu wenye ujuzi na weledi uliostahiki katika kuhakikisha kwamba miradi hii na projects zote ambazo tunazikuta katika mikutano na sehemu mbalimbali zinaletwa Tanzania na kuwafaidisha na kunufaisha Watanzania kwa ujumla wake, ahsante. (Makofi)

Name

Rev. Peter Simon Msigwa

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. MUNDE T. ABDALLAH aliuliza:- Je, Serikali ina mpango mkakati gani kupitia diplomasia ya uchumi na nchi ya China kuunganisha wajasiriamali wadogo, wa kati na wakubwa ili kuingia ubia wa kuimarisha viwanda vidogo na vya kati?

Supplementary Question 2

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, nikushukuru; Mheshimiwa Waziri dhana nzima ya diplomasia ya kiuchumi ni pana sana na hivi karibuni tumeona Tanzania inasita kusaini Mkataba wa EPA pamoja na Jumuiya ya Ulaya. Ni sababu zipi za kimsingi ambazo zinasabisha Tanzania iwe inasuasua, na muda mrefu Wabunge tumekuwa tukiuliza Serikali kwamba haijiandai ku-capitalize kwa fursa zinazotokea? Sasa Mheshimiwa Waziri unasema Serikali imejipanga, ni kwa nini hasa Serikali imekuwa ikisuasua pamoja na kwamba inaweza ikawa na sababu nzuri kusaini huu mkataba pamoja na Jumuiya za Ulaya?

Name

Dr. Susan Alphonce Kolimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Spika, naomba nimjibu kwamba kama tunavyosema kwamba chochote sisi tunachokipigania kama Wizara na kama Serikali ni kwa manufaa ya nchi hii, ni kwa manufaa ya wananchi.
Mheshimiwa Spika, tumesema kwamba hatusaini kwa sababu mkataba ule kwa namna fulani jinsi ulivyokaa uta-affect maslahi ya Tanzania na hasa katika suala zima la kuhakikisha kwamba viwanda vinaweza kuendelea na wewe unajua kuhusu hilo. Kwa hiyo, hatusaini kwa sababu hizo. (Makofi)