Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza:- Je, lini Mradi wa Umwagiliaji wa Kata ya Ikweha uliopo Jimbo la Mufindi Kaskazini utakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa muda wa kuuliza maswali mawili ya nyongeza:-

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa, huu mradi umechukua muda mrefu sana kwenye utekelezaji wake, na Serikali tayari ilikuwa imeshaweka zaidi ya shilingi milioni 800 katika mradi huu. Wananchi wa Mufindi Kaskazini wameusubiri kwa muda mrefu sana. Je, Serikali sasa katika bajeti hii iko tayari kufanya huo upembuzi yakinifu na kuanza ujenzi wa mradi huu? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, utekelezaji wa maagizo ya Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Comrade Chongolo alipotembelea Mradi wa Umwagiliaji wa Ruaha Mbuyuni katika Wilaya ya Kilolo kwa sababu ulikuwa una changamoto kubwa sana? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwenye swali lake la kwanza; ni kweli zmetumika shilingi milioni 800 katika hatua ya awali ambayo kazi yake kubwa ilikuwa ni ujenzi wa banio, njia ndefu ya kilometa 3.5 pamoja na vivuko, lakini katika Mwaka wa Fedha unaokuja tumetenga fedha kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina, ili kupata chanzo cha uhakika cha maji katika skimu hii, ili iweze kufanya shughuli za umwagiliaji mwaka mzima.

Mheshimiwa Spika, jambo hili pia, tulikaa na Mbunge wa jimbo, Mheshimiwa Kigahe, tulizungumza kwa pamoja namna ya kuweza kuboresha skimu hii na hasa katika kuhakikisha kwamba, tunajenga bwawa hilo kwa ajili ya chanzo cha maji cha uhakika.

Mheshimiwa Spika, la pili la kuhusu Ruaha Mbuyuni; tulipokea maelekezo ya Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi na tayari mimi na Mheshimiwa Aweso tulishatuna timu ya wataalamu kwa ajili ya kwenda kuangalia, kufanya marejeo ya usanifu wa eneo lile na hasa kurudisha Mto Lukosi katika njia yake ya asili, ili iweze kusaidia maji yale yaende katika mashamba ya wananchi na yasilete athari. Na hivi sasa kazi inaendelea, naamini baada ya muda mfupi ujao tutapata gharama halisi na utekelezaji utaanza mara moja.

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza:- Je, lini Mradi wa Umwagiliaji wa Kata ya Ikweha uliopo Jimbo la Mufindi Kaskazini utakamilika?

Supplementary Question 2

MHE. MINZA S. MJIKA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Je, ni lini Serikali itajenga Mradi wa umwagiliaji katika Kata ya Mwanyahina katika Jimbo la Meatu?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge alishawasilisha jambo hilo ofisini kwetu na tumekubaliana kwamba, nitawaelekeza wataalam wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kwenda kuangalia lile bwawa lililoko pale kama litakuwa ni chanzo kizuri cha maji kwa ajili ya umwagiliaji. Na baada ya hapo tutawatengea fedha kwenye bajeti inayokuja ili waanze kilimo cha umwagiliaji.

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza:- Je, lini Mradi wa Umwagiliaji wa Kata ya Ikweha uliopo Jimbo la Mufindi Kaskazini utakamilika?

Supplementary Question 3

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona:-

Mheshimiwa Spika, Jimbo la Kalenga lina skimu ambazo ni chakavu sana. Nini mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba, skimu hizo zinafufuliwa na zinakuwa zinahudumia wananchi?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni dhamira ya Serikali kuhakikisha miradi yote ya umwagiliaji inafanya kazi. Ninataka nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba, tunaendelea kuipitia miradi yote, tutakwenda pia katika Jimbo la Kalenga kuangalia na pia, wataalam wetu watafanya kazi tutahakikisha kwamba, miradi hiyo inafanya kazi na wakulima waweze kufanya kilimo cha umwagiliaji.

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza:- Je, lini Mradi wa Umwagiliaji wa Kata ya Ikweha uliopo Jimbo la Mufindi Kaskazini utakamilika?

Supplementary Question 4

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuweza kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, je, Serikali ina mkakati gani wa kutumia vyanzo vya uhakika vya maji kama maziwa na mito kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, tarehe 20 Machi, 2023 mbele ya Mheshimiwa Rais tulisaini mikataba 22 kwa ajili ya kuyapitia mabonde yote ya kimkakati nchi nzima na hasa yale yenye mito na maziwa. Nataka nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge ya kwamba, tumezingatia hoja ya Wabunge humu ndani na tutalitumia Ziwa Victoria, Mto Malagarasi, Mto Ruhuhu, Mto Songwe, kule Litumbandyosi, pamoja na Kilombero, Mto Ngono, Mto Rufiji, hii yote tutaitumia kuhakikisha kwamba, tunafanya kilimo cha umwagiliaji. (Makofi)

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza:- Je, lini Mradi wa Umwagiliaji wa Kata ya Ikweha uliopo Jimbo la Mufindi Kaskazini utakamilika?

Supplementary Question 5

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi ya swali la nyongeza:-

Mheshimiwa Spika, nini mpango wa Serikali kufufua skimu ya umwagiliaji iliyoko Kijiji cha Makangaga, Kata ya Kiranjeranje, Jimbo la Kilwa Kusini?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema pale awali ni dhamiravya Serikali kuhakikisha skimu zote za umwagiliaji zinafanya kazi. Nitashirikiana na Mheshimiwa Mbunge kuangalia kama katika jedwali letu skimu hiyo haipo katika mwaka huu wa fedha, basi tutaitengea fedha kwa ajili ya kuhakikisha kwamba, inafanya kazi na wakulima wanatumia skimu hiyo kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji.

Name

Aleksia Asia Kamguna

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza:- Je, lini Mradi wa Umwagiliaji wa Kata ya Ikweha uliopo Jimbo la Mufindi Kaskazini utakamilika?

Supplementary Question 6

MHE. ALEKSIA A. KAMGUNA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, Jimbo la Malinyi lina maji mengi sana yanayopotea bure. Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha skimu ya umwagiliaji katika Kata ya Malinyi?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, eneo lote la Malinyi linaingia katika mradi huu mkubwa ambao tunaendelea nao wa Bonde la Kilombero na Ifakara Idete. Kwa hiyo, ndani yake humo tutapata nafasi ya kujenga skimu nyingi za umwagiliaji na wabanchi wa Malinyi watanufaika kupitia mradi huu mkubwa unakuja.

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza:- Je, lini Mradi wa Umwagiliaji wa Kata ya Ikweha uliopo Jimbo la Mufindi Kaskazini utakamilika?

Supplementary Question 7

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana:-

Mheshimiwa Spika, katika Kijiji cha Takwa, Kata ya Kinyomshindo, Jimbo la Chemba, kuna skimu ambayo imetelekezwa sasahivi. Siku za nyuma imepata fedha kutoka Serikalini. Ni nini mkakati wa Serikali wa kuifufua skimu ile ya umwagiliaji? Ahsante.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nitahakikisha nashirikiana na Mheshimiwa Mbunge pamoja na wataalam wangu kwa sababu, ipo karibu hapa twende tukaiangalie muda wowote tutakaopata nafasi katikati hapa, ili tuweze kutoa maamuzi sahihi ya utekelezaji wa skimu hii, lakini lengo kubwa la Serikali ni kuhakikisha kwamba, skimu zote zinafanya kazi, ndio dhamira kuu. Kwa hiyo, kama hiyo ndio dhamira kuu maana yake hiyo skimu aliyoitaja ipo ndani ya mpango wa Serikali, baada ya kukaa na wataalamu wetu kuona namna ya kuweza kutekeleza mradi huo.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza:- Je, lini Mradi wa Umwagiliaji wa Kata ya Ikweha uliopo Jimbo la Mufindi Kaskazini utakamilika?

Supplementary Question 8

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana:-

Mheshimiwa Spika, katika jimbo ambalo mimi ndio mwakilishi wao, Halmashauri ya Itigi, kuna skimu moja tu. Je, Serikali sasa iko tayari kuyatumia Mabonde ya Ipalalyo na Bonde la Mnazi kwa ajili ya kutengeneza skimu nyingine?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, tupo tayari na tutashirikiana na Mheshimiwa Mbunge kwa ajili ya kufanya hilo.