Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza: - Je, lini Serikali itapitia Mtaala wa Vyuo Vikuu ili kufungamanisha elimu sambamba na Dira na Mipango ya Maendeleo ya Taifa?

Supplementary Question 1

MHE. NUSRAT S. HANJE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri mno ya Mheshimiwa Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, kwa sababu mradi wa HEET ume-fund vyuo vya umma pekee ambavyo viko 15 kati ya 47 vilivyopo nchini: Ni upi mkakati wa Serikali kuona namna wataweza kuviwezesha vyuo vya private ambavyo kimsingi ni vingi kwa idadi hii ili na vyenyewe viweze kufanya mapitio ya mtaala ili viendane na dira na mwelekeo wa Serikali?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kuna terms of reference zipi ambazo Serikali wameshavipatia vyuo vya private ambavyo waliamua kuanza wenyewe kufanya mapitio, ili sasa kuona namna gani bora tunaweza tukafungamanisha dira na mwelekeo wa Serikali kwenye elimu ambayo inatolewa katika mtaala wa vyuo vikuu nchini? Ahsante.

Name

Prof. Adolf Faustine Mkenda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rombo

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Nusrat Hanje, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza pamoja na kwamba, fedha nyingi zaidi za Mradi wa Higher Education for Economic Transformation zimepelekwa katika vyuo vya umma, bado fedha zimetengwa vilevile kwa ajili ya sekta ya vyuo binafsi kwa mfano, kutoa scholarship, lakini na mafunzo ambayo yanaendeshwa kwa ajili ya kubadilisha mitaala yanachanganya vyuo vyote bila kujali kama ni binafsi ama vya umma.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa TOR; vyuo vyote, kama nilivyosema katika kujibu swali la msingi, vinatengeneza mitaala yao kwanza kwa kupitia kwenye seneti zao, baada ya kukamilisha ndio zinapelekwa kwenye Commission ya Elimu ya Juu kwa ajili ya kupata ithibati. Chuo kinapata kibali cha kuwa chuo kikuu kwa sababu, tunaamini seneti yao ina uwezo mkubwa wa kuidhinisha mitaala. Sasa sisi maelekezo yetu ni kwamba, sasa hivi tuanze kuongeza elimu ya mali na kuzingatia vipaumbele vya nchi, hilo tumeshazungumza na ma-vice chancellors wote wa vyuo vyote na wakati wa kupitisha kwenye ithibati kuna fursa ya sisi kuangalia ni kiasi gani wameji-align na muelekeo huo wa kitaifa.

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza: - Je, lini Serikali itapitia Mtaala wa Vyuo Vikuu ili kufungamanisha elimu sambamba na Dira na Mipango ya Maendeleo ya Taifa?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kunipatia fursa hii kuuliza swali la nyongeza:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imefanya kazi kubwa kujenga vyuo vya VETA sehemu mbalimbali. Je, Serikali ina mkakati gani kufungamanisha mitaala ya vyuo vya VETA na sehemu vilikojengwa? Kwa mfano Kagera tumepata Chuo cha VETA, tunaishukuru Serikali, kufungamanisha mtaala wa VETA na uchumi wa Mkoa wa Kagera kama kusindika kahawa, uvuvi na maeneo mengine kama madini? (Makofi)

Name

Prof. Adolf Faustine Mkenda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rombo

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa kwamba, Vyuo vya VETA vinawaandaa watu kwa ajili ya ajira na kuweza kumudu mazingira ambayo wapo. Na mkakati wa Serikali ni kwamba, pamoja na zile kozi mbalimbali za VETA ambazo kwa kweli zina-cut across kwa mfano kusoma wiring, electrical wiring au mechanics, n.k., lakini kila Chuo cha VETA kinashauriwa kufanya kazi na maeneo yale pale, ili kuchagua baadhi ya masomo ambayo yanakidhi matakwa ya eneo lile ambalo wanafanyia kazi.

Mheshimiwa Spika, najua kwa mfano, chuo ambacho kinajengwa pale Mkuranga kutakuwa na mazungumzo na wanaojenga viwanda katika eneo lile kwa ajili ya kuhakikisha kwamba, mafunzo yanayofanyika pale yanaendana na mahitaji. Kwa hiyo, kadhalika hata cha Kagera na sehemu nyingine tutaendelea kufanya hivyo.

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza: - Je, lini Serikali itapitia Mtaala wa Vyuo Vikuu ili kufungamanisha elimu sambamba na Dira na Mipango ya Maendeleo ya Taifa?

Supplementary Question 3

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kuuliza swali kwamba, zamani tulikuwa na vyuo kama Sokoine kinahusika na kilimo, IFM kilikuwa kinahusika na fedha, Mzumbe inahusika na sheria na utawala, ardhi kinahusika na ardhi, lakini siku hizi kumekuwa na kozi mbalimbali zinazoingia ambazo zinatofautiana na asili ya vyuo hivi. Ni upi mkakati wa Serikali kuona vyuo hivi vinabaki kwenye asili yake, ili tuendelee kuzalisha wataalamu bora zaidi? (Makofi)

Name

Prof. Adolf Faustine Mkenda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rombo

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ni kweli kama alivyosema Mheshimiwa Sanga kwamba, kuna wakati vyuo vilipoanzishwa vilikuwa vina-specialize katika maeneo mbalimbali na vingine kwa kweli, vilikuwa ni taasisi ya elimu ya juu, lakini sio vyuo vikuu kwa tafsiri ambayo tulikuwanayo kwa mfano Mzumbe kilikuwa kinatoa Advanced Diploma badala ya kutoa Degree. Baada ya mageuzi ambayo yalitokea hapo kabla vyote vilipewa vibali vya kuwa vyuo vikuu na hivyo walikuwa wanaweza wakaanzisha programs mbalimbali na wakipata kibali walikuwa wanaendelea kwa hiyo, maana yake hata vyuo kama Sokoine vimeongeza baadhi ya programs nje hata ya eneo ambalo mwanzoni walikuwa wamelizingatia.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, hivyo tuna-insist na tutaendelea kufanya jitihada kuhakikisha kwamba, kila chuo kikuu kinajaribu kuwa na eneo ambalo wame-specialize, ili kuwa na competence kubwa zaidi. Kwa hiyo, kama Sokoine tutatarajia kwamba, waongeze nguvu sana kwenye kilimo, kuna chuo kama Nelson Mandela ambacho kime-specialize kwenye sayansi na teknolojia tungependa wa-focus zaidi kwenye sayansi na teknolojia na kadhalika.

Name

Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza: - Je, lini Serikali itapitia Mtaala wa Vyuo Vikuu ili kufungamanisha elimu sambamba na Dira na Mipango ya Maendeleo ya Taifa?

Supplementary Question 4

MHE. PHILLIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Nataka kumuuliza Mheshimiwa Waziri; huko nyuma imezoeleka mara panapotokea mabadiliko ya mtaala, hizi competence base kwenye madarasa, Serikali inachukua walimu wa Serikali kwenda kuwapa mafunzo kwa ajili ya mabadiliko ya teknolojia, lakini shule za private wanachajiwa na wanalipia. Je, katika huu mtaala mpya unaoendelea sasa Serikali iko tayari kuanza kuunganisha walimu wa private na Serikali ili wawe wanakwenda pamoja kwa sababu, watoto wote ni wa kitanzani?

Name

Prof. Adolf Faustine Mkenda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rombo

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mulugo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kila mitaala inapobadilika Serikali hutenga bajeti kwa ajili ya kuwafundisha walimu kujiandaa kwa ajili ya utekelezaji wa mitaala mipya. Ni kweli kwamba, wakati mwingine fedha ambazo zimekuwa zikitengwa zilikuwa zinakidhi tu kuweza kuwaandaa walimu wa sekta ya umma kwa ajili hiyo na sekta binafsi wanapohudhuria wakati mwingine walikuwa wanachangia au wanajigharamia wenyewe, lakini huduma nyingine wanapewa na Serikali.

Mheshimiwa Spika, tunaongeza jitihada za kuhakikisha kwamba, mabadiliko ya mitaala ambayo yanakuja tutajitahidi kukusanya walimu wote bila kujali wanatoka sekta binafsi au sekta ya umma. Lakini kwa kadiri bajeti itakavyoruhusu tunaweza tukawalipia hata wale wa sekta binafsi. Kama hairuhusu tutawaalika wahudhurie katika semina na mafunzo haya bila kuchajiwa chochote kwa sababu, wale wanaoandaa mafunzo haya na kumbi na gharama za chakula na kila kitu ni ruzuku ya Serikali kwa ajili ya kusaidia vilevile shule binafsi kuandaa walimu wao. Nashukuru.