Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 43 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 565 2023-06-08

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza: -

Je, lini Serikali itapitia Mtaala wa Vyuo Vikuu ili kufungamanisha elimu sambamba na Dira na Mipango ya Maendeleo ya Taifa?

Name

Prof. Adolf Faustine Mkenda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rombo

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Nusrat Shaaban Hanje, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kufanya mapitio ya Sera ya Elimu na Mafunzo ya 2014 na Mitaala katika ngazi ya Elimu ya Awali, Msingi, Sekondari na Mafunzo ya Ualimu. Katika ngazi ya Vyuo Vikuu, kikanuni, mitaala huandaliwa na Vyuo Vikuu vyenyewe kisha kuidhinishwa na Seneti na kuwasilishwa Tume ya Vyuo Vikuu kwa ajili ya uhakiki na ithibati. Hata hivyo, tayari Wizara yangu imeshatoa maelekezo kwa Vyuo Vikuu kuhuisha na kufanya maboresho ya mitaala yote ili iendane na Dira na Mipango ya Maendeleo ya Taifa ambayo kwa sasa inalenga kutoa Elimu itakayompa kijana wa Kitanzania elimu na ujuzi kwa mujibu wa mahitaji ya sasa.

Mheshimiwa Spika, Vyuo Vikuu vya Serikali na Binafsi kupitia mradi wa Higher Education for Economic Transformation (HEET) vimepata mafunzo mbalimbali ya kuandaa programu zinazoendana na vipaumbele vya nchi na mahitaji ya soko la ajira. Aidha, Vyuo vimeunda Kamati za Ushauri wa Insia (Industrial Advisory Committees) zenye Wajumbe kutoka Sekta za Waajiri kwa ajili ya kuzishauri Taasisi za Elimu ya Juu kutoa programu zinazoendana na soko la ajira. Kupitia utaratibu huu, zaidi ya programu 300 zitaanzishwa au kuhuishwa ili kuendana na Dira na Mipango ya Maendeleo ya Taifa sambamba na mahitaji ya sasa ya kijamii, kiuchumi na soko la ajira, ahsante sana.