Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jacquline Andrew Kainja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE K. ANDREA aliuliza:- Je, kuna mpango gani wa kuwapatia vyombo vya usafiri Maafisa Maendeleo ya Jamii ili kufuatilia Mikopo inayotolewa na Halmashauri?

Supplementary Question 1

MHE. JACQUELINE K. ANDREA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, ni pikipiki 85 zilizotoka kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii zimetoka kwa Mikoa 21 na Mkoa wangu wa Tabora zimetoka pikipiki nne. Pikipiki mbili zimeenda Wilaya ya Urambo kwa Kata ya Kazaroho na Uyumbu na zingine zimeenda Kaliua. Sasa Serikali ina mpango gani kuhakikisha inatenga pikipiki nyingi za kutosha kwa ajili ya kuwezesha Afisa Maendeleo, kwa ajili ya kazi hizi za kufatilia mikopo?

Swali la pili, Kanuni ya utoaji mikopo Februari 2021 iliwaagiza Wakurugenzi kutenga pesa 500,000 hadi milioni 5,000, 000 kwa ajili ya ufuatiliaji wa mikopo lakini siyo kila Halmashauri ina uwezo wa kuwa na pesa za kutosha. Swali langu kwa Serikali, haioni kama na Serikali yenyewe ni chanzo cha mikopo hii chefuchefu ambayo tunashindwa kukusanya na kufuatilia vikundi hai na ambavyo siyo hai.

Je, ina mpango gani kuhakikisha sekta hii ya Maafisa Maendeleo ya Jamii wanapata vitendea kazi vya kutosha? Ahsante. (Makofi)

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Jacqueline Kainja, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la kwanza la utengaji wa pikipiki hizi nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba utengaji au upatikanaji wa pikipiki hizi kigezo cha kwanza ni upatikanaji wa bajeti. Kwa hiyo, kama Serikali tutaendelea kutenga bajeti ili tuweze kuwafikia wananchi wote ikiwezekana Kata zote au Wilaya zote za Mkoa wa Tabora.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili kwamba Halmashauri nyingine hazina uwezo wa kutenga pesa kwa ajili ya kupeleka Maafisa wetu kwenda kuangalia au kufuatilia vikundi hivyo. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kuwa haya pia ni maelekezo ya Serikali kwamba Wakurugenzi wote katika Halmashauri zote wahakikishe kwamba wanaendelea kutenga fedha kama ambavyo imeelekezwa na wale ambao watashindwa maelekezo yetu ni kwamba wawasiliane na Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa ajili ya kuona ni jinsi gani tunatatua tatizo hilo. (Makofi)