Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 43 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 560 2023-06-08

Name

Jacquline Andrew Kainja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE K. ANDREA aliuliza:-

Je, kuna mpango gani wa kuwapatia vyombo vya usafiri Maafisa Maendeleo ya Jamii ili kufuatilia Mikopo inayotolewa na Halmashauri?

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jacqueline Kainja Andrea, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa vyombo vya usafiri kwa ajili ya Maafisa Maendeleo ya Jamii ili kuwawezesha kufanya kazi kwa ufanisi.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuboresha kwa kuwawezesha usafiri na kutenga pesa kati ya 500,000 mpaka 5,000,000 kwa ajili ya ufatiliaji kama ilivyoelekezwa kwa mujibu wa kanuni ya ufatiliaji wa mikopo ya makundi haya yakiwemo ya wanawake, vijana na walemavu.

Mheshimiwa Spika, katika Mwezi Februari, 2023, Serikali iligawa pikipiki 916 kwa Watendaji wa Kata, pikipiki 85 kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii, pikipiki 5, 889 kwa Maafisa Ugani wa Kilimo na pikipiki 1,200 kwa Maafisa Ugani wa Mifugo.

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kusisitiza kwamba utumiaji wa vyombo hivyo kwa pamoja ndiyo utatuletea tija katika kufikia maendeleo ya kufuatilia vikundi vyetu na misaada inayoendelea kupelekwa katika zile asilimia 10. Nashukuru. (Makofi)