Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza:- Je, lini Serikali italeta mradi wa kuhifadhi Mazingira katika chanzo cha maji cha Mto Ruaha na shamba la miti la Sao Hill?

Supplementary Question 1

MHE. DAVID M. KIHENZILE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza. Moja; kwa kuwa wananchi wa Mufindi Kusini wameamua kuwa na shughuli mbalimbali mbadala ili wasikate miti na kuharibu vyanzo vya maji. Je, Serikali iko tayari sasa kuwaunga mkono na itaanza lini kuchimba mabwawa ili waweze kufanya shughuli zingine mbadala kama za uvuvi katika eneo la Mufindi Kusini?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuzingatia unyeti na uzito na umuhimu mkubwa wa Mto Ruaha kwenye Taifa letu. Je, Serikali iko tayari kufanya elimu kwenye Mamlaka za Serikali Mitaa ili itoe fursa kwa wananchi kujua pengine umuhimu wa kuhifadhi mto huo?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa David Kihenzile, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na uchimbaji wa mabwawa katika maeneo aliyoyataja Mheshimiwa Mbunge. Kwanza nimpongeze kwa sababu alishiriki katika hili kuona kwamba tafiti inakamilika na kupita Bodi ya Maji ya Bonde la Mto Rufiji, tafiti ile Mheshimiwa Mbunge imeshakamilika na tunatarajia mwaka ujao wa fedha tuweze kuchimba mabwawa maeneo yale ambayo tunaona yatakuwa ni msaada kwa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile kwa suala la fedha kwa ajili ya kuendeleza semina mbalimbali kutoa elimu kwa jamii; kama nilivyojibu kwenye jibu langu la msingi, tayari sisi kama Wizara tumeanza kutoa elimu kwa hasa viongozi wa vyombo vya watumia maji, lakini sasa hivi tutakwenda zaidi kwa viongozi na makundi mbalimbali na jukumu hili litatekelezwa na Bonde la Rufiji.